PICHA 9: IGP Sirro alivyofunga mafunzo ya Maafisa Uhamiaji leo CCP, Moshi
Share
1 Min Read
SHARE
Leo June 24, 2017 Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro alikuwa Mgeni rasmi katika sherehe ya kufunga mafunzo ya Maafisa wa Uhamiaji waliomaliza Kozi Namba Moja, sherehe zilizofanyika Chuo cha Polisi Moshi, CCP.
Hizi hapa picha 9 kutoka katika sherehe hizo ambapo Kozi hiyo ilihusisha Warakibu Wasaidizi, Wakaguzi Wasaidizi, Sajini Meja, Sajentina Koplo.
IGP Simon Sirro akikagua Gwaride la Maafisa wa Uhamiaji wakati wa sherehe za kumaliza kozi namba moja kwa Maafisa hao
IGP Simon Sirro (kulia) akibadilishana mazungumzo na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala baada ya kukagua Gwaride wakati wa sherehe za kumaliza Kozi ya Kwanza ya Maafisa wa Uhamiaji, CCP Moshi
IGP Simon Sirro akiwahutubia Maafisa Uhamiaji baada ya kukagua Gwaride wakati wa sherehe za kumaliza kozi ya kwanza kwa Maafisa UhamiajiIGP Simon Sirro akimvisha Cheo Mkaguzi Msaidizi Hadija Masoud Ali wakati wa sherehe za kumaliza kozi ya kwanza ya Maafisa Uhamiaji katika Chuo cha Polisi Moshi, CCP.
ULIIKOSA HII?? Jeshi la Polisi DSM limejipanga kuhakikisha amani inatawala wakati wa Sikukuu ya Eid El Fitr…bonyeza PLAY kwenye VIDEO hii hapa chini kutazama!!!