Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Mstaafu Kikwete kwenye orodha moja na Bill Gates, Dangote na Ellen Johnson Sirleaf
Share
Notification Show More
Latest News
Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta
September 22, 2023
Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou
September 22, 2023
Xavi kuongeza mkataba wa Barcelona hadi 2025
September 22, 2023
Kuelekea fainali ya polisi jamii DPA cup mashabiki wajigamba afisa michezo atoa neno
September 22, 2023
Nigeria:Tinubu aidhinisha nyongeza ya mishahara kwa Taasisi za Elimu ya Juu za Shirikisho
September 22, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Mix > Mstaafu Kikwete kwenye orodha moja na Bill Gates, Dangote na Ellen Johnson Sirleaf
Mix

Mstaafu Kikwete kwenye orodha moja na Bill Gates, Dangote na Ellen Johnson Sirleaf

January 23, 2017
Share
3 Min Read
SHARE
Kazi ya millardayo.com na AyoTV siku zote ni kukusogeza karibu na matukio yote kutoka kwenye kona mbalimbali za dunia ambapo kwenye post hii nakukutanisha na hii ya Rais Mstaafu wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
 ______________________________
Dr. JK ameshiriki katika uzinduzi wa baraza la kutokomeza Malaria Duniani (End Malaria Council) uliofanyika tarehe 19 January 2016 huko Davos Uswisi ambapo baraza la kutokomeza Malaria linaundwa na Wajumbe 9 ambao ni watu mashuhuri katika sekta ya umma na sekta binafsi duniani na orodha yenyewe ya Wajumbe ndio hii hapa chini
 ______________________________
1. Bill Gates – Mwanzilishi na mmiliki wa Bill Gates Foundation
2. Ray Chambers – Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malaria
3. Peter Chermin –Mwanzilishi wa Chermin  Entertainment na Chermin Group
4. Aliko Dangote – Rais na Mtendaji Mkuu wa Dangote Group
5. Idrisa Deby –Rais wa Chad kwa nafasi yake ya Mwenyekiti wa Taasisi ya ALMA
6. Jakaya Kikwete –Rais Mstaafu wa Tanzania
7. Graca Machel – Mwanzilishi wa Foundation for Community Development,Msumbiji
8. Luis Alberto Moreno –Rais wa Inter-American Development Bank
9. Ellen Johnson Sirleaf – Rais wa Liberia.
______________________________
Rais mstaafu Jakaya Kikwete akisalimiana na Bill Gates ambaye mpaka January 2017 jina lake limetajwa kuwa ndio anashika namba 1 kwa utajiri duniani

Lengo la Baraza hilo ni kuunganisha nguvu za wadau na mataifa duniani kukabiliana na hatimaye kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria ifikapo mwaka 2030 ambapo kuanzishwa kwa Baraza hilo kumetokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika vita dhidi ya malaria katika miaka 15 iliyopita.
 _____________________
Katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika Davos, Baraza hilo limejadili kuhusu upatikanaji wa rasilimali za kutosha za kuwezesha kutoa msukumo katika upatikanaji wa vifaa tiba, dawa, tafiti na uvumbuzi wa mbinu na nyenzo za kisasa za kuzuia, kupambana na hatimaye kutokomeza ugonjwa wa Malaria katika nchi za Afrika, Asia na Amerika ya Kusini.
J.K Ray Chambers na Bill Gates

Baada ya uzinduzi wa Baraza hilo, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete ambaye utotoni kwake alipoteza kaka yake kwa ugonjwa wa  Malaria pamoja na ndugu wengine wengi kaika maisha yake alisema >>> ” Kutokomeza Malaria iliwahi kuwa ndoto isiyotekeleza lakini sasa kuifikia ndoto hiyo ni dhahiri…..tunawea kuifanya Malaria kuwa historia na kuutokomeza ugonjwa huu katili katika uso wa dunia“.

Rais mstaafu Jakaya Kikwete na Ray Chambers
Tanzania ni moja ya nchi zinazosifika barani Afrika na duniani kwa kuweza kupiga hatua kubwa katika kutokomeza ugonjwa wa Malaria. Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, takwimu zinaonyesha kuwa maambukizi ya malaria yamepungua kwa asilimia 70 na vifo vimepungua kwa asilimia 50.

ULIPITWA? Makomando walivyoonyesha uwezo mbele ya Rais Magufuli? bonyeza hapa chini kutazama kwenye hii video

You Might Also Like

Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta

Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou

Xavi kuongeza mkataba wa Barcelona hadi 2025

Kuelekea fainali ya polisi jamii DPA cup mashabiki wajigamba afisa michezo atoa neno

UN yaitaka Iran kuachana na sheria mpya kuhusu hijab

TAGGED: TZA HABARI
Millard Ayo January 23, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Miji 20 duniani ambako Baiskeli zimetumika zaidi kuliko Magari
Next Article Nay wa Mitego kaikamilisha studio yake, kuna hizi video fupi katupa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta
Sports September 22, 2023
Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou
Sports September 22, 2023
Xavi kuongeza mkataba wa Barcelona hadi 2025
Sports September 22, 2023
Kuelekea fainali ya polisi jamii DPA cup mashabiki wajigamba afisa michezo atoa neno
Top Stories September 22, 2023

You Might also Like

Sports

Arsenal haihitaji motisha ya ziada dhidi ya Spurs- Arteta

September 22, 2023
Sports

Derby ya London Kaskazini huko Arsenal ni ‘changamoto kubwa’ – Postecoglou

September 22, 2023
Sports

Xavi kuongeza mkataba wa Barcelona hadi 2025

September 22, 2023
Top Stories

Nigeria:Tinubu aidhinisha nyongeza ya mishahara kwa Taasisi za Elimu ya Juu za Shirikisho

September 22, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?