Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Walichosema Watanzania walioshinda Bajaj kutoka SportPesa
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
March 26, 2023
Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”
March 26, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Walichosema Watanzania walioshinda Bajaj kutoka SportPesa
Top Stories

Walichosema Watanzania walioshinda Bajaj kutoka SportPesa

November 6, 2017
Share
4 Min Read
SHARE

Promosheni ya SHINDA NA SPORTPESA inaingia siku ya 12 ambapo tayari washindi 11 wameshapatikana na zoezi la kukabidhi bajaji hizo likiendelea, watanzania wa rika zote kutoka kila kona ya Tanzania wameendelea kushiriki kikamilifu na kujishindia zawadi zao kutoka kwenye promosheni hiyo ambayo itadumu kwa siku 100 tangu ilipozinduliwa rasmi Oktoba 25 mwaka huu.

Kwa wiki nzima sasa, SportPesa imekuwa ikiingia mtaa kwa mtaa kutoa bajaji hizo aina ya TVS KING huku washindi husika wakielezea furaha zao sambamba na matumizi ya bajaji hizo.

Kubashiri hakuishii hapa

Cassian Anthony, mwalimu wa Shule ya Msingi Ngwelo wilayani Lushoto-Tanga alikuwa ni mshindi wa bajaji ya pili na aliamua kufunga safari kutoka Lushoto kuja kukabishiwa bajaji yake jijini Dar katika maeneo ya Kimara ambapo baba yake mdogo anaishi.

“Mzigo huu utafanyia kazi hapa hapa Dar ndio maana nimetumia nauli kutoka Tanga nimekuja hapa japokuwa niliambiwa mzigo naletewa kule lakini nikasema niufuate huku huku.

“Kwa kifupi nitaitumia kufanya biashara na kile kidogo ninachopata najua sasa hivi kitaongezeka, kwahiyo utakapoona vitu kama vile ujue hii ni nguvu ya SportPesa.

Kubashiri na SportPesa hakuishii hapa, kwasababu TVS KING zipo 100 naweza nikapata hata tano ila mara nyingine nikija tena hapa basi ujue ni kwa ajili ya Jackpot ile zaidi ya Milioni 200

Nilikatisha darasa

SportPesa pia ilitinga mitaa ya Mbagala Kibulugwa kukabidhi bajaji kwa Hussein Iddi Balo ambaye alikuwa mshindi wa bajaji ya tano, ambaye naye alitoa lake la moyoni.

“Wakati napigiwa simu nilikuwa kwenye shughuli zangu za taaluma. Nilishtushwa sana hadi darasa lenyewe nikalisitisha

“Nimejisikia furaha sana baada ya kubashiri na SportPesa ambapo niliweka mechi za Real Madrid, Everton na Southampton lakini nikapiga ndege wawili kwa jiwe moja, nimekosa kule lakini nikafanikiwa kushinda Bajaji aina ya TVS KING

Niliona masihara

Naye Joseph Mallya kutoka Himo, Kilimanjaro alikuwa ni mshindi wa bajaji ya nne na hakuona haja ya kusubiri aletewe kule kule alipo, akaamua kufunga safari ili kuja kukabidhiwa mzigo wake hapa hapa.

“Nimekuja hapa SportPesa kufuatilia ile bajaji ya TVS KING ambayo niliambiwa nimeshinda kwasababu sikuamini kwahiyo nikaamua nije mwenyewe kufuatilia.

“Nawashauri watu waendelee kucheza na SportPesa, kwasababu mimi mwenyewe kwanza niliona masihara lakini sasa hivi ndio naamini kama ni kweli na inabidi sasa nifanye biashara ya kusafirisha abiria.

Naye Sudi Mkwara kutoka Gongolamboto anakuwa mshindi wa bajaji ya nane. Sudi ambaye ni askari polisi wa kituo cha Kurasini anaamua kukabidhi mzigo kwa mzee wake ambaye anajishughulisha na uuzaji wa Samaki wakati ambao yeye atakuwa safarini kikazi.

“Kwakweli sikuamini kama ningeweza kushinda TVS KING kutoka SportPesa kwasababu najua wanaoshiriki ni wengi sana na hivi vitu vinategemea bahati zaidi.

“Mimi nasafiri kesho (Jumamosi) kikazi kwahiyo Bajaji hii nitamuachia baba yangu hapa nyumbani ambaye atakuwa anaisimamia na kitakachopatikana basi kitatumika kwa ajili ya kusomesha wanangu ambao ni wajukuu zake.

Jinsi ya kushiriki promosheni

Ili kushiriki kwenye promosheni hii ya SHINDA TVS KING NA SPORTPESA, kwanza kabisa unatakiwa kujisajili kwa kutuma neno GAME kwenda 15888 (kama bado hujajisajili), weka pesa kwa namba ya biashara 150888 kisha piga *150*87# au tembelea www.sportpesa.co.tz kuweka utabiri wako mara nyingi.

Ukishaweka utabiri wako, utatumiwa ujumbe unaokutaka kutuma neno SHINDA kwenda 15888 ili kuingia kwenye droo. Kadri unavyocheza mara nyingi ndivyo unajiongezea nafasi ya kushinda kila siku.

Manara kabeba TV na kuja nayo kwa Waandishi leo kuonyesha Simba inavyoonewa (+video)

You Might Also Like

Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM

Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’

Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake

Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza limefanya misa Takaridu ya Kumuombea Hayati JPM

TAGGED: habaridaily
Rama Mwelondo TZA November 6, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Balaa la Alikiba kwenye stage ya Fiesta Dodoma
Next Article MAHAKAMANI: Yaliyojiri leo kesi ya Aveva na Kaburu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
Magazeti March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
Top Stories March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
Top Stories March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
Top Stories March 26, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM

March 26, 2023
Top Stories

Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’

March 26, 2023
Top Stories

Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”

March 26, 2023
Top Stories

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza limefanya misa Takaridu ya Kumuombea Hayati JPM

March 26, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?