Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Kamati ya kudumu ya Bunge ya nishati na Madini yaridhishwa na kasi ya Maendeleo ya Mradi huu
Share
Notification Show More
Latest News
Video: RC Shigella atoa tamkoa kufuatia Wananchi kuchoma kituo cha Polisi
April 1, 2023
Machinga wa Tegeta wafunguka ‘Usafi ni tatizo sokoni, tumepokea vifaa vya Milioni 5’
April 1, 2023
Picha: Maafisa habari washuhudia maboresho ya Miundombinu, mifumo katika bandari ya DSM
April 1, 2023
Picha: Mwenyekiti wa CCM Dkt Samia aongoza kikao maalum cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM
April 1, 2023
Jeshi la Zimamoto na uokoaji lapokea magari mapya matatu ya kuzima moto, Waziri Bashungwa anena haya
April 1, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Kamati ya kudumu ya Bunge ya nishati na Madini yaridhishwa na kasi ya Maendeleo ya Mradi huu
Top Stories

Kamati ya kudumu ya Bunge ya nishati na Madini yaridhishwa na kasi ya Maendeleo ya Mradi huu

March 17, 2023
Share
3 Min Read
SHARE

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imefanya ziara katika kituo cha kupokea na kupoza umeme mkubwa wa kilovoti 400/220/132/33 cha Chalinze mkoani Pwani pamoja na njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka katika mradi wa bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere (JNHPP) kuja katika kituo hiki ili kujionea maendeleo ya ujenzi wa miradi hii inayotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kuwataka Wizara ya Nishati pamoja na TANESCO kuhakikisha wanakamilisha kwa wakati miradi hii miwili kabla ya kukamilika kwa mradi wa bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere (JNHPP).

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dustan Kitandula (Mbunge) alipokuwa akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya Kamati hiyo.

Mhe. Kitandula amesema kamati imeridhishwa na utekelezaji wa mradi hiyo na kuongeza kuwa itasaidia sana katika uwekezaji mkubwa na kukuza uchumi wa nchi yetu.

“Uchumi wa nchi unakuwa kwa kasi sana sambamba na mahitaji ya upatikanaji wa umeme hivyo TANESCO hakikisheni mnaweka msukumo mkubwa kwenye miradi hii” alisema Mhe. Kitandula.

Kwa Upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato amesema kukamilika kwa mradi huu wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze ambao unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia mia moja utanufaisha Mikoa mbalimbali kwa kuongeza hali ya ubora na uhakika wa upatikanaji wa Umeme wa uhakika utakaoingizwa katika Gridi ya Taifa.

Aidha, Mhe. Byabato ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuidhinisha fedha za kugharamia miradi hii ambapo hapo awali mradi huu wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze ulikuwa ufadhiliwe na mradi wa North Grid kabla ya Serikali kuamua kuanza kuufadhili mradi huo kwa asilimia mia moja.

.

Naye Meneja mradi wa kituo hiki cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze, Mhandisi Newton Livingstone amesema kuwa mradi huu unajumuisha miradi miwili ambayo ni njia ya kusafirisha umeme mkubwa kutoka bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere (JNHPP) hadi kituo Cha chalinze kwa msingi wa kilovoto 400 yenye urefu wa kilomita 160 wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 51.5 na shilingi bilioni 39.12 pamoja na kituo cha kupokea na kupoza umeme mkubwa wa kilovoti 400/220/132/33 cha Chalinze wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 44.06 na shilingi bilioni 30.85 kitakachohusisha ufungaji wa mashine umba sita zenye uwezo wa Megavoti 250 kila moja.

Ujenzi huu wa mradi wa kituo cha kupokea na kupoza umeme cha Chalinze kwa sasa umefikia asilimia 59 wakati ambapo kwa upande wa njia ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka JNHPP umefikia asilimia 92.

You Might Also Like

Video: RC Shigella atoa tamkoa kufuatia Wananchi kuchoma kituo cha Polisi

Machinga wa Tegeta wafunguka ‘Usafi ni tatizo sokoni, tumepokea vifaa vya Milioni 5’

Picha: Maafisa habari washuhudia maboresho ya Miundombinu, mifumo katika bandari ya DSM

Picha: Mwenyekiti wa CCM Dkt Samia aongoza kikao maalum cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM

Jeshi la Zimamoto na uokoaji lapokea magari mapya matatu ya kuzima moto, Waziri Bashungwa anena haya

Edwin TZA March 17, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Rapa Snoop Dogg azindua lebo yake mpya ya kahawa “INDOxyz”
Next Article Watu saba waburuzwa Mahakamani kisa vurugu mgodini Mirerani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Video: RC Shigella atoa tamkoa kufuatia Wananchi kuchoma kituo cha Polisi
Top Stories April 1, 2023
Machinga wa Tegeta wafunguka ‘Usafi ni tatizo sokoni, tumepokea vifaa vya Milioni 5’
Top Stories April 1, 2023
Picha: Maafisa habari washuhudia maboresho ya Miundombinu, mifumo katika bandari ya DSM
Top Stories April 1, 2023
Picha: Mwenyekiti wa CCM Dkt Samia aongoza kikao maalum cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM
Top Stories April 1, 2023

You Might also Like

Top Stories

Video: RC Shigella atoa tamkoa kufuatia Wananchi kuchoma kituo cha Polisi

April 1, 2023
Top Stories

Machinga wa Tegeta wafunguka ‘Usafi ni tatizo sokoni, tumepokea vifaa vya Milioni 5’

April 1, 2023
Top Stories

Picha: Maafisa habari washuhudia maboresho ya Miundombinu, mifumo katika bandari ya DSM

April 1, 2023
Top Stories

Jeshi la Zimamoto na uokoaji lapokea magari mapya matatu ya kuzima moto, Waziri Bashungwa anena haya

April 1, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?