Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema hatua ya Halmashauri ya Tunduma kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 4.6 kwa vikundi 150, ikiwa ni mikopo ya Halmashauri ya asilimia 10 itokanayo na mapato ya ndani kwa ajili ya vikundi vya wananwake, vijana na watu wenye Ulemavu ni utekelezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyeelekeza Halmashauri zote nchini kuanza kutoa mikopo hiyo kwa kutumia mfumo mpya wa utoaji na usimamizi wa mikopo hiyo.
Aliongea hayo wakati akikagua miradi ya maendeleo mkoani Songwe, Mhe. Kikwete amebainisha kuwa katika kuhakikisha mikopo hiyo inakuwa na tija kwa Walengwa Mhe. Rais Samia alielekeza kupitia na kuboresha utoaji wa mikopo hiyo ambapo baada ya kukamilika maboresho hayo, dirisha la utoaji mikopo lilifunguliwa rasmi mwezi Septemba 2024.
Aidha, amesema katika uongozi wa Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan katika kipindi chake amejitahidi kuhakikisha vijana wanafunguliwa fursa na kuwezeshwa, maelekezo yake hayo yamekuwa yakifanyiwa kazi na Halmashauri, Serikali Kuu,hivyo amevitaka vikundi kutumia fedha hizo kwenye miradi yenye tija na kurejesha kwa wakati ili na wengine wanufaike na mikopo hiyo.
Katika hatua nyingine Mhe.Kiwete amekagua na kuweka jiwe la msingi katika miradi ya Ujenzi wa majengo ya Hospitali ya Halmashauri ya Momba,