Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Ahukumiwa kuchapwa viboko 24
Share
Notification Show More
Latest News
Jorginho aondoka Chelsea na kusaini Arsenal
February 1, 2023
Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain
January 31, 2023
Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza
January 31, 2023
Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)
January 31, 2023
Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg
January 31, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Ahukumiwa kuchapwa viboko 24
Top Stories

Ahukumiwa kuchapwa viboko 24

November 28, 2022
Share
2 Min Read
SHARE

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ileje mkoani Songwe imemhukumu mkazi wa kijiji cha Msia kata ya Chitete wilayani humo, Furaha Simkonda achapwe viboko 24 baada ya kumkuta na hatia ya kutaka kumbaka mwanafunzi wa darasa la kwanza mwenye umri wa miaka sita.

Hakimu Mfawidhi wa mahakama hiyo, Shughuli Mwampashe alisema mahakama imemtia hatiani mshitakiwa huyo mwenye umri wa miaka 18 baada ya kujiridhisha na ushahidi wa upande wa mashitaka.

Mwampashe alisema mahakama ilitoa hukumu ya kuchapwa viboko 24 kwa mujibu wa kifungu cha sheria 160(B) cha sura ya 17 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2019.

Alisema vitendo vya ubakaji na ulawiti vimeshamiri wilayani humo hivyo adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa wenye tabia za kuharibu ndoto za watoto.

Simkonda aliomba impunguzie adhabu kwa kuwa ilikuwa mara ya kwanza kufanya kosa kama hilo na atakuwa balozi mwema kwenye jamii.

Awali, mwendesha mashitaka wa serikali, Elibariki Mpinga aliieleza mahakama kuwa kijana hiyo alitenda kosa Julai 8 mwaka huu kwa kumvamia mwanafunzi huyo majira ya saa tano asubuhi wakati akienda shuleni akiwa amevaa sare za shule.

Mpinga alidai wakati mshitakiwa akitaka kumfanyia kitendo cha kingono mtoto huyo, mwananchi aliyesikia kelele kichakani alikwenda kumuokoa mtoto.

Mahakama ilielezwa kuwa kijana huyo alikamatwa Julai 24 mwaka huu katika eneo la sokoni kwenye Kijiji Cha Msia kwa ushirikiano na wananchi baada ya kuwapo taarifa kuhusu kijana huyo kutaka kumnajisi mtoto.

Mmoja wa mashahidi katika kesi hiyo, Esinati Mtinya, aliieleza mahakama kuwa wakati akienda shambani alisikia sauti kichakani ya mtoto kulia na alipokwenda, alikuta kijana huyo amemuangusha akiwa amevua suruali mpaka kwenye magoti na alijaribu kumkamata lakini alimshinda nguvu na kukimbia.

Nje ya mahakama, Ofisa Ustawi wa Jamii wilayani humo, Tabitha Swila alisema vitendo vya ubakaji vimekithiri wilayani humo na kwamba, kesi zaidi ya tano zimefikishwa mahakamani hapo zikiwamo za kunajisi watoto wenye umri chini ya miaka 15.

You Might Also Like

Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain

Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza

Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)

Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg

Biden akataa kutuma ndege za kivita Ukraine

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA November 28, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo November 28, 2022
Next Article Mchimba madini akamatwa kwa mauaji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Jorginho aondoka Chelsea na kusaini Arsenal
Sports February 1, 2023
Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain
Top Stories January 31, 2023
Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza
Top Stories January 31, 2023
Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)
Top Stories January 31, 2023

You Might also Like

Top Stories

Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain

January 31, 2023
Top Stories

Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza

January 31, 2023
Top Stories

Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg

January 31, 2023
Top Stories

Biden akataa kutuma ndege za kivita Ukraine

January 31, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?