List ya makocha 10 wa soka wanaotajwa kupokea mshahara mkubwa zaidi.
Share
2 Min Read
SHARE
List ya makocha wa mpira wa miguu wanaoongoza kwa kulipwa vizuri kwenye soka mpaka sasa ambapo namba 1 imechukuliwa na Pep kama unavyoona list nzima hapa chini
1. Pep Guardiola
Huyu ni kocha wa Bayern Munich, ameitumikia timu yake kwa mafanikio makubwa huk akiisaidia kupata mataji mbalimbali, ndiye kocha anayeongoza kwa kulipwa mshahara mkubwa kuliko wote kwa kupokea kiasi cha dola milioni 24
2. Jose Maourinho
Huyu ni kocha wa Chelseaambaye anajulikana kwa kuwa na maneno mengi,kwa sasa yupo mbioni kuwania ubingwa wa ligi kuu ya England, ni kocha anashika nafasi ya pili kwa kulipwa kiasi kikubwa cha pesa na hupokea kiasi cha dola milioni 17.
3. Marcello Lippi
Ana mchango mkubwa kwenye Timu ya Taifa ya Italy na kufanikiwa kutwaa kombe la dunia mwaka 2006, anapokea kiasi cha dola milioni 14.
4. Fabio Capello
Huyu ni kocha wa timu ya Taifa ya Russia, anapokea kiasi cha dola milioni 13
5. Carlo Ancelotti
Huyu ni kocha mkuu wa Real Madrid, anapokea kiasi cha dola milioni 10.5.
6. Arsene Wenger
Amekuwa kocha wa Arsenaltoka mwaka 1996, na anapokea kiasi cha dola milioni 10.
7. Gerardo Martino
Huyu ni kocha wa Argentina, anapokea kiasi cha dola milioni 7.5.
8. Jurgen Klopp
Huyu ni kocha wa Borrusia Dortmund, anapokea kiasi cha dola milioni 6.
9. Manuel Pellegrini
Huyu ni kocha wa Manchester City, anapokea kiasi cha dola milioni 5.75.
10. Jorge Jesus
Huyu ni kocha wa klabu ya Beneficatangu mwaka 2009, anapokea kiasi cha dola milioni 5.5
Nitaendelea kukupatia kila stori inayonifikia mtu wangu, niko tayari kukutumia wakati wowote kupitia Twitter, Instagram na Facebook ukijiunga na mimi kwa kubonyeza >>>twitterInstaFacebook