RAIS DK.Samia Suluhu Hassan ameipongeza Kampuni ya Oryx Gas pamoja na wadau wengine kwa kuendelea kushiriki kikamilifu katika kampeni ya nishati safi ya huku akitoa rai ya wadau hao kupeleka gesi katika maeneo ya vijijini.
Ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la Oryx Gas wakati wa uzinduzi wa kampeni ya matumizi nishati safi ya kupikia Kitaifa iliyozinduliwa katika viwanja vya Jitegemee wilayani Muheza mkoani Tanga.
“Mitungi ya gesi inapoisha inabaki ndani kama feniture (Samani za ndani) ,hivyo nimeomba sekta binafsi na nimekutana na Oryx Gas pamoja na wadau wengine wakanihakikishia wataendelea kuipeleka mitungi ili wananchi waendelee kutumia.”amesema Rais Samia huku akiipongeza Oryx Gas.
Awali akitoa maelezo kwa Rais Samia, Meneja Miradi ya Nishati Safi ya Kupikia kutoka Oryx Gas Tanzania Peter Ndomba amesema kampuni hiyo imekuwa ikifanya jitihada mbambali za kuunga mkono kampeni ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini na
mkakati wao ni kuona kila nyumba inakuwa na mtungi wa gesi ya kupikia.
“Tunamshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa ajenda yake ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Oryx Gas tumekuwa wadau wakubwa na tumefanya jitihada nyingi tokeo ilipotangazwa kama ajenda rasmi ya nchi kwamba wananchi tuanze kutumia nishati safi ya kupikia
“Tumeongeza miundombinu ya kusambaza mitungi ya Oryx Gas hasa katika maeneo ya vijiji ambapo kwa sasa huwezi kuikosa Oryx gas. mitungi ya Oryx inapatikana kila miji,Wilaya na vijijini pia tupo .Pia tumekuwa tukishiriki katika shughuli za mbalimbali za kuwezesha ukuaji wa matumizi ya nishati safi ambapo tumeweza kuisaidia jamii mbalimbali ikiwemo ya Wanawake kwa kuiwezesha kufikia hayo malengo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan (kushoto) akızungumza na maofisa wa Kampuni ya Oryx Gas Tanzania baada ya kufika katika banda la Oryx wakati wa uzinduzi wa kampeni ya matumizi ya nishati safi kitaifa uliofanyika katika Viwanja vya CCM Jitegemee wilayani Muheza mkoani Tanga.Rais yuko Mkoani Tanga kwa ziara ya kikazi