Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: EACOP yafanya jambo kulinda makaburi ya kimila Igunga
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 3, 2023
June 3, 2023
Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’
June 2, 2023
Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi
June 2, 2023
Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.
June 2, 2023
Nyota wa zamani wa Manchester United Lingard kuondoka Nottingham Forest
June 2, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > EACOP yafanya jambo kulinda makaburi ya kimila Igunga
Top Stories

EACOP yafanya jambo kulinda makaburi ya kimila Igunga

March 22, 2023
Share
3 Min Read
SHARE

Kampuni ya Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP Ltd) kwa kuheshimu mila na desturi za watu walioguswa na mradi (PAPs) imesaini mkataba wa kusimamia haki na kuheshimu tamaduni za Wazawa (FPIC) na jamii ya Wataturu wanaoishi katika kijiji cha Mwamayoka katika Wilaya ya Igunga, Tanzania kwa ajili ya kuchepusha njia ili kuyalinda makaburi yao ya kimila

Awali Wataturu hao walikuwa na wasiwasi wa kuathiriwa  kwa makaburi yao yaliyopo eneo la Bung’enda na maeneo yao mengine kadhaa ya kuabudia endapo mradi ungeanza ujenzi.

Akizungumza wakati wa sherehe ya kusaini makubaliano hayo, Mkurugenzi  Mkuu wa EACOP Tanzania Wendy Brown amesema baada ya majadiliano na jamii na viongozi wa kimila, EACOP ilifanya mapitio ya kiufundi na kukubali kupitisha bomba hilo katika njia mpya ili kutokuwa na athari yoyote katika maeneo yao muhimu ya mila na kiutamaduni.

Bi. Wendy Brown amesema, EACOP inaheshimu haki na mila za makundi yote ya kikabila yanayoguswa na mradi.

Hivyo, amesema  EACOP itaendelea kushirikiana na jamii zote zilizoguswa na mradi pamoja na viongozi wao wa kimila ili kuhakikisha kuwa maoni yao yamezingatiwa wakati wote wa kupanga na kutekeleza mradi.

Mkataba huu wa FPIC ni wa pili kusainiwa na EACOP baada ya kusaini mkataba kama huo hapo awali na jamii ya Akie inayoishi Kanda ya Kaskazini.

Amesema kusainiwa kwa mikataba hii ni kielelezo tosha kuwa mradi wa EACOP unashirikisha makundi yanayoguswa katika ngazi zote za utekelezaji wake na kuheshimu mila, tamaduni na haki za jamii husika.

Ameongeza mradi wa EACOP unatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, jamii na utunzaji wa mazingira.


Gesuda Masanja, ambaye ni chifu wa jumuiya ya Wataturu alipongeza hatua ya EACOP kwa kuzingatia mila zao, akisema kuwa mradi huo utasaidia kwa maendeleo ya jamii yake.

Akizungumza awali, Martha Bayo, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Igunga, pia alipongeza hatua ya EACOP na kuitaka jamii ya Wataturu kuwa walinzi wa bomba hilo la mafuta ghafi litakapokamilika.

Lucas Bugota, ambaye ni Diwani wa Kata ya Igunga pia ameusifu mradi wa EACOP kwa hatua hiyo, akisema jamii ya Wataturu wameweka historia katika kulinda mila na tamaduni zao.

Nailejileji Tipap kutoka Jukwaa la Wafugaji lisilokuwa la Kiserikali (Pingos) alisema hatua ya kampuni ya  EACOP kusaini mkataba wa FPIC inalinda maslahi ya jamii ya Wataturu hao.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo (DAS) Godlove Kawiche aliihakikishia kampuni ya EACOP  juu ya dhamira ya serikali ya kutekeleza mradi wa bomba hilo la mafuta ghafi.

Pia aliipongeza timu ya wataalam wa EACOP  kwa kushirikisha jamii zilizoathiriwa katika mchakato mzima wa ujenzi wa bomba hilo.

 

You Might Also Like

Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’

Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi

Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.

Serikali ya Congo na mahakama ya ICC zakubaliana kuimarisha ushirikiano

Amnesty yaonya Iran dhidi ya Kunyonga kwa Kesi zinazohusiana na madawa ya kulevya

TAGGED: habari daily
Rama Mwelondo TZA March 22, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Simba yaandika historia Ligi ya Mabingwa Afrika
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 22, 2023
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 3, 2023
Magazeti June 3, 2023
Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’
Top Stories June 2, 2023
Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi
Top Stories June 2, 2023
Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.
Top Stories June 2, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’

June 2, 2023
Top Stories

Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi

June 2, 2023
Sports

Nyota wa zamani wa Manchester United Lingard kuondoka Nottingham Forest

June 2, 2023
Top Stories

Serikali ya Congo na mahakama ya ICC zakubaliana kuimarisha ushirikiano

June 2, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?