Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Nyumba za Mabilionea zenye thamani zaidi Duniani…nyumba ya Bill Gates je?
Share
Notification Show More
Latest News
Picha: Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris awasili nchini Ghana
March 27, 2023
Kenya:Mmoja auawa kwa kupigwa risasi kwenye vurugu za maandamano kisumu.
March 27, 2023
Katibu Tawala msaidizi Mkoa wa Morogoro awaagiza hili watumishi wa Halmashauri za Wilaya
March 27, 2023
Aliyemzushia DAS taarifa za uongo Jela kifungo Mwaka mmoja
March 27, 2023
Waziri Nape kufungua Mkutano wa Wahariri Mkoani Morogoro
March 27, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Nyumba/ Mijumba > Nyumba za Mabilionea zenye thamani zaidi Duniani…nyumba ya Bill Gates je?
Nyumba/ Mijumba

Nyumba za Mabilionea zenye thamani zaidi Duniani…nyumba ya Bill Gates je?

July 31, 2017
Share
5 Min Read
SHARE

Uwezo wa watu kuishi unategemea namna ya utajiri au uwezo wa kifedha waliokuwa nao. Wanavyoingiza fedha zaidi ndivyo wanavyozidi kubalika katika namna ya kuishi. Wapo matajiri ambao hujenga nyumba ambayo kutokana na ukubwa wake inaweza kuishi hadi watu 100 na huwatumia wabunifu wa hali ya juu…

Hii hapa Top Ten ya nyumba ghali zaidi za Mabilionea

10: 360 Mountain Home Road

Nyumba hii ipo Westside, California, Marekani na inamilikiwa na Masayoshi Son, CEO wa Softbank. Kasri hili limejengwa kwa namna yake likiwa na bwawa na kuogelea la futi 1.117, uwanja wa tennis, Maktaba. Kwa sasa linakadiriwa kuwa na thamani ya Dollar Milioni 117.5 zaidi ya Tsh. Bilioni 258.

9: Xanadu 2.0

Hii inapatikana Seattle, Washington na inamilikiwa na Bill Gates, mwasisi-mwenza na Mwenyekiti wa Microsoft. Lina eneo la futi 66,000 likisanifiwa kwa mtindo wa Pacific lodge – lina maktaba binafsi, chumba cha chakula, bwawa la kuogelea ambalo lina mfumo wa muziki chini (swimming pool with underwater music system). Linakadiriwa kuwa na thamani ya Dollar Milioni 120.5 zaidi ya Bilioni 264.

8: Blossom Estate

Ukitembelea Palm Beach, Florida, utakutana na kasri hili ambalo linamilikiwa na Kenneth Griffin, Mwasisi na CEO wa Citadel LLC. Jengo kwenye ekari 8 ambalo linajumuisha nyumba nne zinazojitegemea katika eneo ambapo tatu kati ya hizo zinaangalia ufukwe. Lina thamani ya Dollar Milioni 130 zaidi ya Tsh. Bilioni 286.

7: Ellison Estate

Jumba hili linapatikana Woodside, California, ni milki ya Tajiri namba tatu katika nchi ya Marekani, Larry Ellison, mwasisi-mwenza wa Oracle Corporation. Kuna majengo 10 ndani ya ekari 23, bwawa la samaki, Ziwa lililotengenezwa, chumba cha chai, na nyumba ya bafu ambayo imesanifiwa kwa mtindo wa Kijaan. Thamani yake ni Dollar Milioni 200 zaidi ya Tsh Bilioni 440.

6: One Hyde Park

Nyumba ya ukubwa wa futi 25,000 ambayo ipo katika jiji la London, inamilikiwa na tajiri wa Ukraine, Rinat Akhtemov. One Hyde Park ni moja kati ya makazi maarufu sana United Kingdom. Thamani yake ni Dollar Milioni 213 zaidi ya Tsh. Bilioni 468.

5: 18-19 Kensington Palace Gardens

Nayo pia iko katika jiji la London, ikimilikiwa na Lakshmi Mittal, mmilikiwa wa viwanda vya kutengeneza chuma wa India. Ina vyumba 12 vya kulala, bafu la Kituruki, eneo la kuegesha magari zaidi ya 20. Wakati wa kununuliwa ilikuwa ndiyo nyumba iliyouzwa kwa bei ya juu zaidi Duniani. Awali lilimilikiwa na Berne Ecclestone, Mkuu wa Formula One ambapo thamani yake kwa sasa ni Dollar Milioni 222 ambazo ni zaidi ya Tsh. Bilioni 488.

4: Four Fairfield Pond

Hii ipo Sagaponack, New York na inamilikiwa na Ira Rennert, mwekezaji wa Marekani na Mfanyabiashara. Jumba hili lina vyumba 29 vya kulala, mabafu 39, na mabwawa 3 ya kuogelea na umeme wa kijitegemea. Thamani yake ni Dollar Milioni 248.5 zaidi ya Tsh. Bilioni 545.

3: Villa Leopolda

Kasri hili lipo Villefranche-sur-Mer, Ufaransa, likienea katika eneo la ukubwa wa ekari 18 na lilitumika kama makazi ya King Leopold II wa Ubelgiji lakini sasa linamilikiwa na Mbarazil Lily Safra ambaye amerithi baada ya kifo cha mumewe Edmond Safra. Thamani yake ni Dollar Milioni 750 zaidi ya Tsh. Trilioni 1.65.

2: Antillia

Linajulikana pia kama ‘One Billion Dollar home’, lipo katika eneo la ukubwa wa square foot 400,000 katika mji wa Mumbai, India na linamilikiwa na Bilionea Mukesh Ambani. Kutokana na ukubwa wake linahitaji watu 600 kulihudumia. Kama linavyoitwa jumba hili lina thamani ya Dollar Bilioni 1 zaidi ya Tsh. Trilioni 2.2.

1: Buckingham Palace

Kasri linamilikiwa na familia ya kifalme na kwa sasa lina thamani ya Dollar Bilioni 1.55 zaidi ya Tsh. Trilioni 3.3. kasri hili lina jumla ya vyumba 775.

UTAJIRI WA BAKHRESA: Hoteli ya kisasa anayojenga baharini Zanzibar…tazama kwenye video hii hapa chini!

You Might Also Like

PICHA 10:Unahitaji Nyumba au kupanga Mikocheni, Palm Village wana habari njema

VIDEO: Jionee Jengo refu DSM, apartment zake simchezo zinaanzia Million 250

Kutoka Donge Tanga kwa Mzee Majuto hizi hapa PICHA 20

PICHA 23: Kutoka kwenye kilele cha Mbio za Mwenge, Zanzibar

ZANZIBAR! Kilele Mbio za Mwenge itakuwa katika Uwanja huu (+Picha 17)

TAGGED: Mijengo, nyumba, Pichaz, Top 10
Millard Ayo July 31, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Sababu za CHADEMA kwa nini fedha haipatikani mifukoni (+Video)
Next Article CHADEMA kuhusu hali ya Uchumi wa nchi, imetaja vigezo vitano
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Picha: Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris awasili nchini Ghana
Top Stories March 27, 2023
Kenya:Mmoja auawa kwa kupigwa risasi kwenye vurugu za maandamano kisumu.
Top Stories March 27, 2023
Katibu Tawala msaidizi Mkoa wa Morogoro awaagiza hili watumishi wa Halmashauri za Wilaya
Top Stories March 27, 2023
Aliyemzushia DAS taarifa za uongo Jela kifungo Mwaka mmoja
Top Stories March 27, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris awasili nchini Ghana

March 27, 2023
Top Stories

Kenya:Mmoja auawa kwa kupigwa risasi kwenye vurugu za maandamano kisumu.

March 27, 2023
Top Stories

Katibu Tawala msaidizi Mkoa wa Morogoro awaagiza hili watumishi wa Halmashauri za Wilaya

March 27, 2023
Top Stories

Waziri Nape kufungua Mkutano wa Wahariri Mkoani Morogoro

March 27, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?