Hali ya Ugonjwa wa Corona Tanzania, Waziri ummy aweka wazi idadi ya wagonjwa (+video)
June 1, 2020
Share
1 Min Read
SHARE
Waziri Ummy Mwalimu amesema kuwa, idadi ya wagonjwa wa Corona hapa nchini imepungua kwa kiasi kikubwa na kubaki na wagonjwa wanne pekee walio katika Mkoa wa DSM.
Waziri Ummy ameyabainisha hayo leo June 1, 2020, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ya uzinduzi wa jengo la Bodi ya Mkonge lililopewa jina la Mkonge House, na kusisitiza kuwa kwa takwimu hizi watu wasijisahau, bali waendelee kujikinga na ugonjwa huo.
“Hapa Tanga hatuna mgonjwa wa Corona, DSM katika Hospitali ya Amana wamebaki 3, Mloganzila 1, Kibaha hatuna mgonjwa, Mwanza hatuna mgonjwa jambo la kusisitiza ni kuwa Corona bado ipo tuendelee kujikinga, na mimi nilisema pale Ikulu Dodoma katika Uwaziri wangu sikuwahi kupitia kipindi kigumu kama hiki cha Corona kwakweli nilihenya” Waziri Ummy.
IGP SIRRO AKERWA NA WAFUNGWA WALIOSAMEHEWA NA RAIS, AZUNGUMZIA UCHAGUZI