Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Kachumbari yasababisha Mume kumuua Mke Tanzania
Share
Notification Show More
Latest News
Waziri Dr Damas Ndumbaro na Rais TFF watinga AVIC Town kuzungumza na wachezaji wa Yanga SC
September 29, 2023
Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu
September 29, 2023
Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA
September 29, 2023
Mohbad: Polisi wa Lagos wamkamata Sam Larry ahusishwa na kifo cha Mohbad
September 29, 2023
Reece James kurejea kikosoini hivi karibuni- Chelsea
September 29, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Magazeti > Kachumbari yasababisha Mume kumuua Mke Tanzania
Magazeti

Kachumbari yasababisha Mume kumuua Mke Tanzania

January 20, 2017
Share
3 Min Read
SHARE

Kila asubuhi mimi Millard Ayo nazisogeza karibu yako habari zote kubwa kutoka kwenye Magazeti mbalimbali ya Tanzania ambapo huwa naziweka kwenye page ya Twitter ya @millardayo na kwenye Youtube ya millardayo na millardayo.com.

Moja ya habari iliyoandikwa kwenye magazeti ya leo January 20 2017 ni pamoja na hii ya kwenye gazeti la Mtanzania, yenye kichwa cha habari ‘Mume aua mke kisa kachumbari’ 

#MTANZANIA Stella Ibrahim adaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na mume wake Daniel, sababu yatajwa kuwa kachumbari iliyochacha pic.twitter.com/Cnd80lgPeN

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

Gazeti hilo limeripoti kuwa mkazi wa Mtaa wa Mageuzi, Manispaa ya Shinyanga, Stella Ibrahim (39), anadaiwa kuuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na mume wake, Ibrahim Daniel kwa kile kilichoelezwa  kuwa alipewa kachumbari iliyochacha.

Tukio hilo limetokea juzi usiku, baada ya Daniel kumshushia kipigo mkewe akidai kuwa alimpa kachumbari ambayo haikuhifadhiwa vizuri na mboga nyingine aliyodai haina kiwango.

Mashuhuda wa tukio hilo, walidai kuwa Daniel alifika nyumbani akiwa amelewa, kisha kuulizia  kachumbari ambayo alikula jana, ndipo mtoto wake, Elizabeth Ibrahim (13) akamwonesha kachumbari  ambayo inadaiwa tayari ilikuwa imechacha.

Walisema hakufurahia kuona kachumbari hiyo imeharibika, ndipo alipoanza kuuliza kwanini haikuhifadhiwa vizuri, akisimulia mkasa huo, mtoto wa marehemu, Daniel Ibrahim (12) alisema baba yeke alifika nyumbani saa moja usiku, alimkuta yeye akiwa na mdogo wake, Elizabeth aliyemuhoji kwanini kachumbari imeharibika, lakini hakupata jibu.

‘Baada ya kuingia ndani, baba alimuuliza Elizabeth kachumbari aliyoiacha (Januari 16, mwaka huu) iko wapi, akaoneshwa. Baada ya kuiangalia aliiona imechacha, alitoka nje na kuchukua fimbo ambayo huwa anaiweka juu ya nyumba na kutaka kuanza kumpiga, kabla ya kuanza kumpiga Elizabeth alikimbia.;-Mtoto wa marehemu

“Baada ya Elizabeth kukimbia, mama ambaye alikuwa kazini alifika nyumbani, akamkuta baba akifoka, akauliza kuna nini, baba akasema kwanini hakupika mboga yenye kiwango na kwanini ulipikwa ugali mwingine wakati  kulikuwa na ugali uliobaki mchana’;- Mtoto wa marehemu 

Alisema kutokana na maswali hayo, mama yake alimjibu kwa hasira kwanini hakuacha fedha nyumbani za kununulia mboga yenye kiwango anachotaka.

‘Baada ya baba anayedaiwa alikuwa amelewa kudai kachumbari yake, mama aliingilia kati, akajikuta anaambulia kipigo… vipimo vya daktari vinaonyesha alipigwa na kitu kizito kwenye utosi, kichwa kikavimba na damu kavujia ndani kwa wingi’;-Mwenyekiti wa mtaa

#NIPASHE Serikali imesisitiza kuwa wizara zote zinatakiwa kuwa zimehamia Dodoma kabla ya February 28 na hakuna mabadiliko yoyote pic.twitter.com/itmxrPorBF

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#NIPASHE Wakati matukio ya ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi yakipungua, hali imebadilika na sasa watu hufukua makaburi ya albino pic.twitter.com/AyOKWPTkYv

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#NIPASHE Serikali imezifunga maabara 117 za watu binafsi mkoani Geita baada ya kuthibitika kutokuwa na sifa pic.twitter.com/RegwyzYdU5

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#NIPASHE Kamati ya bunge imeiagiza TPA kuhakikisha bandari ya Tanga inajiendesha ili kuipatia serikali mapato badala ya kutegemea ruzuku pic.twitter.com/t7SknnmI0S

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#JamboLEO Lissu akana mahakamani kuchapisha taarifa za uchochezi, zenye kichwa cha habari 'machafuko yaja Z'bar' asema yeye si mchapishaji pic.twitter.com/AWyhNBEcWX

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#MTANZANIA Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA yasema kwasasa matukio ya ujangili yamepungua nchini tofauti na miaka iliyopita pic.twitter.com/R5kUVxx6vw

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#HabariLEO Serikari imewasilisha pendekezo la mabadiliko ya sheria ya bodi ya mikopo ili kuwezesha wanafunzi wa diploma kupewa mikopo pic.twitter.com/4gMkmjtsHe

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#MTANZANIA 79% ya wahitimu elimu ya juu nchini hawana ujuzi wa kufanya kazi ktk soko la ajira la kimataifa, husoma kwa nadharia bila vitendo pic.twitter.com/dOYdrNhtb1

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#HabariLEO Zaidi ya mil 41 zilizotolewa na TASAF kwa ajili ya kunusuru kaya maskini Bunda zadaiwa kutafunwa na viongozi waliopewa kusimamia pic.twitter.com/6JxV3imTGp

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

#NIPASHE BAWACHA kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya sheria kuhusu uhalali wa Rais Magufuli kuteua wabunge wawili wanaume wiki hii pic.twitter.com/rlahQKLxRA

— millardayo (@millardayo) January 20, 2017

AyoTV MAGAZETI: Vilio Mgodi mkubwa nchini kufungwa,Wanaosoma diploma kupewa mikopo, Bonyeza play hapa chini 

You Might Also Like

Habari kubwa Magazetini Kenya leo September 29, 2023

Habari kubwa Magazetini Kenya leo September 28, 2023

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 28, 2023

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 27, 2023

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 25, 2023

TAGGED: magazeti
Edwin Kamugisha TZA January 20, 2017
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article AyoTVMAGAZETI: Vilio Mgodi mkubwa nchini kufungwa,Wanaosoma diploma kupewa mikopo
Next Article Baada ya Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu nae kapata timu Ulaya
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Waziri Dr Damas Ndumbaro na Rais TFF watinga AVIC Town kuzungumza na wachezaji wa Yanga SC
Sports September 29, 2023
Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu
Top Stories September 29, 2023
Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA
Top Stories September 29, 2023
Mohbad: Polisi wa Lagos wamkamata Sam Larry ahusishwa na kifo cha Mohbad
Entertainment September 29, 2023

You Might also Like

Top Stories

Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

September 29, 2023
Top Stories

Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA

September 29, 2023
Sports

Reece James kurejea kikosoini hivi karibuni- Chelsea

September 29, 2023
Top Stories

Rais wa Urusi Vladimir Putin akutana na kamanda mkuu wa zamani wa Wagner Group

September 29, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?