Kupitia usaili wa nchi nzima, Safari Lager imegundua kizazi kipya cha mabingwa wa mpira wa miguu wa Tanzania – timu ya Mabingwa ya Safari Lager Cup. Wakiwa na ujuzi, shauku, na hamasa ya ushindi, wachezaji hawawaligunduliwa kwenye Kombe la Kwanza la Safari Lager.
Mashindano haya yalipita katika mikoa mikuu, yakifanya usailiMbeya, Arusha, Mwanza, na Dar es Salaam ili kuwapatawanasoka vijana wenye vipaji na wanaoonesha moyo wa mpirawa miguu wa Kitanzania. Baada ya mashindano makali na kambi za mafunzo kali chini ya makocha bora, wachezaji 64 walijitokeza na kuchuana katika nafasi ya kuwa mabingwa.
Mabingwa hawa wanatoka katika nyanja mbalimbali za maishalakini wanashirikiana kwa bidii, kujitolea kwa timu, na hamasakubwa ya kuandika majina yao katika historia ya michezo:
Abubakary Lyanga – GK (Dar es Salaam), Edmund Zephania – GK (Arusha), Steven Claudia – RB (Mwanza), Benson Burton – RB (Dar es Salaam), David Siraji – LB (Arusha), MathiasAnthony – LB (Dar es Salaam), Kisumo Anthony – CB (Mwanza), Jeremiah James – CB (Mbeya), Baraka Thobias – WB (Mbeya), Augostino Anderson – LB (Arusha) and SomjiHailonje – CAM (Mbeya).
Samson Kamese – CAM (Mbeya), Festo Mkumbo – RW (Mbeya), Salim Shida Ally – RW (Mbeya), Jacob Mussa Ndege– CM (Mbeya), Hussein Ally – CM (Dar es Salaam), Kelvin Komba – ST (Mbeya), Habib Kingo – ST (Dar es Salaam), Ibrahim Samweli – FW (Arusha), Erick Ponsian – FW (Arusha), Marwa Mwita – LW (Mwanza) and Prince Paul – WB (Arusha)
Safari ya Timu ya Mabingwa Wapya wa Soka ya Safari Lager ndio imeanza tu. Sasa wanaanza kambi ya mafunzo ya wiki tatuchini ya magwiji wa mchezo, wakipata ujuzi wa juu hukuwakionekana katika vyombo vya habari vya kitaifa wakijiandaakwa mechi moja kubwa ya Mwisho itakayokua ya kihistoria.
“Zaidi ya michuano, Kombe la Safari Lager linajumuishahamasa ya Kitanzania isiyoyumba,” alisema Pamela Kikuli, Meneja Chapa wa Safari Lager. “Tunajivunia sana kuzinduatimu hii ambayo imepitia changamoto na mchuano mkali ili kuthibitisha ubora wao. Watanzania wote wanapaswa kuwaungamkono na kuwatambua kama alama za matumaini kwa vijanawengine.”
Katika safari ya kupanda katika ubingwa, timu hii inaoneshauvumilivu wa kufuata ndoto dhidi ya vikwazo vyote. Hadithiyao ya kishujaa inaanza sasa – ishuhudie kwa kufuatilia page za Safari Lager