Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: KSIJ na Ibrahim Hajj kila mwaka wanachangia Unit 400 za damu
Share
Notification Show More
Latest News
Breaking: William Ruto atangazwa kuwa Rais Kenya, Shangwe na furaha zaibuka mitaani Nairobi
August 15, 2022
Matokeo ya Urais Kenya kutangazwa leo, Mgombea Ruto awasili Ukumbini Boma ‘Kusubiria matokeo hayo’
August 15, 2022
Live: Matokeo ya Urais nchini Kenya yanatangazwa muda huu
August 15, 2022
Manara na Wana-Yanga wakomaa kuwa kejeli Simba ‘Mlete Mzunguu’
August 15, 2022
Club ya Wolves ya England kuleta makocha wawili Tanzania
August 15, 2022
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > KSIJ na Ibrahim Hajj kila mwaka wanachangia Unit 400 za damu
Top Stories

KSIJ na Ibrahim Hajj kila mwaka wanachangia Unit 400 za damu

August 30, 2021
Share
4 Min Read
SHARE
Mtaalam wa Maabara kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama Kanda ya Mashariki, Gisbert Ruseneka, akimtoa damu, mmoja wa waumini wa Juimuiya ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJ), wakati wa kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha kiongozi wa dhehebu hilo Imamu Hussein, kwenye msikiti wa KSIJ jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa waumini wa Juimuiya ya Khoja Shia Ithnasheri Jamaat (KSIJ) akishiriki katika zoezi la uchangiaji damu wakati wa kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha kiongozi wa dhehebu hilo Imamu Hussein, kwenye msikiti wa KSIJ jijini Dar es Salaam.
Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi la uchangiaji damu lilioandaliwa na Jumuiya Khoja Shia kwa kushirikiana na Taasisi ya Ibrahim Hajj.

WANACHAMA wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna-Asheri Jamaat (KSIJ) kwa kushirikiana na Taasisi ya Ibrahim Hajj, wamejitolea kuchangia damu kwa Mpango wa Taifa wa Damu Salama, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Imamu Hussein.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto, alihudhuria hafla hiyo ya uchangiaji damu, iliyofanyika Msikiti wa KSIJ katikati ya jiji, ambako aliwapongeza  Wana Jumuiya hao kwa kudumisha utamaduni chanya wa kusaidia wenye uhitaji ikiwemo uchangiaji damu huo.

Meya Kumbilamoto alibainisha kuwa, KSIJ na Ibrahim Hajj, wameionesha jamii ya Watanzania namna wanavyopaswa kujitoa kwa ustawi wa maisha wenye uhitaji, na kwamba damu iliyochangwa na Wana Jumuiya hao, inaenda kuokoa maisha Wengi miongoni mwa wahanga wa ajali, wamama wajawazito na wagonjwa wa kansa ya damu.

Kumbilamoto aliwapongeza KSIJ na Ibrahim Hajj na kuzitaka taasisi zingine na jamii kuiga utamaduni chanya unaofanywa na wanachama hao, ambao unalenga sio tu kuakisi yalivyokuwa maisha ya kiongozi wao Imamu Hussein, bali kuunga mkono jitihada za Serikali katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wake.

“Nitoe wito kwa jamii, kuiga mfano wa KSIJ na Ibrahim Hajj, ambao wamekuwa wakijitolea damu kila mwaka. Awali walikuwa wakitoa mara moja kwa mwaka kila wanapokuwa na maadhimisho haya, lakini Sasa wamekuwa wakichangia damu kila wanapoombwa kufanya hivi.

“KSIJ na Ibrahim Hajj, wameenda mbali zaidi kwa Sasa kwa kujitosa katika utatuzi wa changamoto mbalimbali, hasa zinazoikabili sekta ya Elimu na Afya nchini, walikotoa vifaa tiba, vifaa vya elimu na hata ujenzi na maboresho ya miundombinu kwenye Sekta hizo muhimu kwa maendeleo ya jamii,” alisisitiza Meya Kumbilamoto.

Akizungumza kwa niaba ya KSIJ, Ain Sharrif, ambaye ni Mwanachama Mwandamizi Jumuiya hiyo, alisema utamuduni huo wa kuchangia damu wamekuwa wakiufanya kila (Mwezi Muharram) wanapoadhimisha kifo cha kiongozi wao Sayyidina Hussein (Imamu Hussein), aliyekufa kwa kujitoa mhanga yapata miaka 1400 iliyopita.

“Tumekuwa tukifanya hivi tangu mwaka 2008, lengo likiwa ni kuyaishi maisha ya Imamu Hussein, ambaye alisimama imara katika kujitolea kwa ustawi wa maisha ya aliowaongoza na jamii iliyomzunguka. Nasi tunafanya haya na mengineyo ili kufuata nyayo zake na kutii wosia zake.

“Leo tunavyo vituo vitatu vinavyochangia damu jijini Dar es Salaam, ambapo pia kupitia Hospitali ya Ibrahim Hajj tumekuwa tukisaidia mamia ya watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu kwa kuwapatia misaada mbalimbali kulingana na mahitaji yao, sambamba na huduma za matibabu,” alisema Sharrif.

Naye Mtaalamu wa Maabara ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Samuel Mluma, aliishukuru KSIJ na Taasisi ya Ibrahim Hajj kwa kuthamini na kuijali jamii ya wenye uhitaji na kujitolea kuchangia damu, ambayo mahitaji yake ni makubwa.

“Kila mwaka KSIJ na Ibrahim Hajj wamekuwa wakichangia zaidi ya Unit 400 za damu kupitia maombolezo yao haya ama tunapowahitaji.

“Mahitaji nchini ni makubwa, takribani chupa 250,000 kwa mwaka, kwahiyo tunapowapata watu na Taasisi za mfano wa Kama KSIJ na Ibrahim Hajj, tunakuwa na uhakika wa makusanyo ya kutosha kukidhi mahitaji,” alisema Mluma

You Might Also Like

Breaking: William Ruto atangazwa kuwa Rais Kenya, Shangwe na furaha zaibuka mitaani Nairobi

Matokeo ya Urais Kenya kutangazwa leo, Mgombea Ruto awasili Ukumbini Boma ‘Kusubiria matokeo hayo’

Live: Matokeo ya Urais nchini Kenya yanatangazwa muda huu

Azikwa akiwa hai huko Madaba, DC afika eneo la tukio, ‘Jambo hili ni la kinyama’

Rais Samia atoa Bilioni 15 jimboni kwa Shigongo

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA August 30, 2021
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article “Suala la kujenga nchi la kwetu sote” Rais Samia (+picha)
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 30, 2021
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Breaking: William Ruto atangazwa kuwa Rais Kenya, Shangwe na furaha zaibuka mitaani Nairobi
Top Stories August 15, 2022
Matokeo ya Urais Kenya kutangazwa leo, Mgombea Ruto awasili Ukumbini Boma ‘Kusubiria matokeo hayo’
Top Stories August 15, 2022
Live: Matokeo ya Urais nchini Kenya yanatangazwa muda huu
Top Stories August 15, 2022
Manara na Wana-Yanga wakomaa kuwa kejeli Simba ‘Mlete Mzunguu’
Sports August 15, 2022

You Might also Like

Sports

Club ya Wolves ya England kuleta makocha wawili Tanzania

August 15, 2022
Sports

Inter Milan wawapa Yanga cha kusema, Shaffi Dauda atia neno, Manara apigilia msumari

August 15, 2022
Sports

Barbara awatuliza mashabiki wa Simba, wataka Mzungu aachwe wana mashabiki na mbinu za Kocha

August 15, 2022
Sports

Aziz Ki Mfalme mpya town, mchezo dhidi ya Simba SC ya dhihirissha ubora wake, ‘Jemedari amwagia sifa’

August 14, 2022
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?