Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: VIDEO: Rais Magufuli amteua mrithi wa Jaji Lubuva
Share
Notification Show More
Latest News
Picha: Diamond ameingia makubaliano ya kudhamini mashindano ya Ndondo Cup
August 19, 2022
Kuelekea Sensa Agosti 23, Mbunge wa Jimbo la Ushtu anena hili kwa Wananchi wake
August 19, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 19, 2022
August 19, 2022
Kiwanda cha Chai Mponde Ujenzi wake umefikia 95%
August 18, 2022
Ajali ya Basi yaua watano Singida, Polisi azungumza hali ya Majeruhi
August 18, 2022
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > AyoTV > VIDEO: Rais Magufuli amteua mrithi wa Jaji Lubuva
AyoTV

VIDEO: Rais Magufuli amteua mrithi wa Jaji Lubuva

December 22, 2016
Share
2 Min Read
SHARE

Leo December 22 2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jaji Semistocles Kaijage kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Jaji Semistocles Kaijage ameteuliwa kuongoza Tume hiyo kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia December 20 2016. Jaji Semistocles Kaijage anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu Damiani Lubuva ambae muda wake wa kuwa Mwenyekiti umemalizika rasmi mnamo tarehe 19 Desemba, 2016.

Aidha, Rais Magufuli amemteua  Jaji Mstaafu Hamid Mahamoud Hamid kuwa Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kipindi kingine cha miaka 5 kuanzia tarehe 20 Desemba, 2016. Jaji Mstaafu Hamid Mahamoud Hamid alikuwa Makamu Mwenyekiti wa NEC na amemaliza kipindi chake cha kwanza cha miaka 5 mnamo tarehe 19 Desemba, 2016.

Rais Magufuli pia amemteua Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Jaji Harold Reginald Nsekela kuwa Kamishna wa Maadili katika Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia tarehe 20 Desemba, 2016. Jaji Mstaafu Nsekela anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Salome S. Kaganda ambae amestaafu mnamo tarehe 10 Desemba, 2016.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amewateua Majaji 4 wa Mahakama Kuu kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani kuanzia leo tarehe 22 Desemba, 2016 kama ifuatavyo:-

⦁  Jaji Dkt. Gerald Ndika
⦁  Jaji Jackobs Mwambegele
⦁ Jaji Rehema Kiwanga Mkuye
⦁ Jaji Sivangilwe Sikalalilwa Mwangesi

Wateule wote waliotajwa katika taarifa hii wataapishwa kesho Ijumaa, tarehe 23 Desemba, 2016 saa 3:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

VIDEO: Humphrey Polepole baada ya kukutana na Rais Magufuli, Bonyeza play hapa chini kutazama

You Might Also Like

Picha: Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais akutana na Waandishi wa Habari Ikulu DSM

Rais Samia amjibu Zitto ombi lake kumuachia Mbowe “Kusameheana kupo” (video+)

Rais Samia akishiriki katika maadhimisho ya miaka 50 ya Kongamano la wachungaji

Live:Rais Samia Suluhu Hassan akizindua chanjo ya Covid-19 Ikulu DSM

Video:Majaji wa Bongo Star Search wafunguka kwenye fainali usiku huu

TAGGED: Ikulu, Rais Magufuli
Edwin Kamugisha TZA December 22, 2016
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article VIDEO: Onyo la polisi msimu huu wa sikukuu
Next Article U HEARD: Maneno ya Nay wa Mitego kwa Nisha baada ya kufeki mimba
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Picha: Diamond ameingia makubaliano ya kudhamini mashindano ya Ndondo Cup
Entertainment August 19, 2022
Kuelekea Sensa Agosti 23, Mbunge wa Jimbo la Ushtu anena hili kwa Wananchi wake
Top Stories August 19, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 19, 2022
Magazeti August 19, 2022
Kiwanda cha Chai Mponde Ujenzi wake umefikia 95%
Mix August 18, 2022

You Might also Like

Mix

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 17, 2022

August 17, 2022
Mix

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 13, 2022

August 13, 2022
MixTop Stories

Mwana FA alivyoungana na Viongozi mbalimbali kuhamasisha Zoezi la Sensa, Masuguru Wilayani Muheza

August 11, 2022
Mix

Bwawa la Mwalimu nyerere sasa kazi ni Usiku na Mchana, ‘kukamilika June 2024’ Waziri Makamba anena

August 9, 2022
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?