Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Maadhimisho ya siku ya nyuki kitaifa kufanyika Mkoani Katavi
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 26, 2023
March 26, 2023
Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mayanja atoa maagizo haya kwa Wakulima Wilayani humo
March 25, 2023
Gigy Money katuletea hii video mpya ‘ogopa’ itazame hapa
March 25, 2023
Picha: Polisi Jamii Cup yazinduliwa Mkoani Manyara
March 25, 2023
Mkurugenzi wa Asas afunguka, ‘Tunawafugaji Elfu 6500, Rungwe na Isanu Busokelo uzalishaji ni mkubwa’
March 25, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Maadhimisho ya siku ya nyuki kitaifa kufanyika Mkoani Katavi
Top Stories

Maadhimisho ya siku ya nyuki kitaifa kufanyika Mkoani Katavi

May 12, 2022
Share
3 Min Read
SHARE

Watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho ya siku ya Nyuki duniani ambayo kitaifa yatafanyika katika wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi tarehe 21 Mei 2022 ili kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu umuhimu wa mdudu nyuki katika maisha ya kila siku ya mwanadamu na mazingira yake.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii nchini Mhe Balozi. Dkt.Pindi Chana (Mb) kwenye taarifa yake kwa waandishi wa Habari Jijini Dodoma.

Waziri Chana ameeleza chimbuko la maadhimisho haya ni azimio la Baraza la Umoja wa Mataifa la Tarehe 20 Desemba, 2017 lililoazimia kuwa tarehe 20 Mei, ya kila mwaka, kuwa ni siku ya nyuki duniani.

Kwa lengo kuu la kutambua mchango wa mdudu huyu katika kukuza usalama wa chakula na uhifadhi wa mazingira duniani.

“Kufuatia azimio hilo, kila nchi inajukumu la kuadhimisha siku hiyo kuendana na mazingira yake, ili kuendelea kujenga uelewa kwa jamiii juu ya umuhimu wa mdudu nyuki. Na hii ndiyo sababu, sisi kama nchi, tunaungana na dunia kufanya maadhimisho haya kwa mara ya tatu tangu yalipoanzishwa miaka mitano (5) iliyopita”- Waziri Chana

Akitaja manufaa ya mdudu Nyuki, Waziri Chana amesema ni pamoja na chakula na dawa, kujipatia fedha za ndani na kigeni, ajiri zaidi ya watu milioni 2 katika mnyororo mzima wa thamani itokanayo na sekta ya ufugaji wa Nyuki.

“Wizara ina mikakati ya kuhakikisha sekta hii inaajiri zaidi ya watu milioni 2.5 ifikapo 2031. Aidha, manufaa yatokanayo na nyuki ni mengi zaidi ya ajira, kwani hata chakula tunachokula nyuki ni sehemu ya wachavushaji wakubwa, na hivyo kutuhakikishia upatikanaji wa chakula”. Aliongeza Waziri Chana

Kauli mbiu ya mwaka huu wa 2022 ni “Nyuki wamehusika: Harakati za kujikwamua upya zisisahau nyuki” (Bee engaged: Build back better for bees).

Kauli mbiu hii imekuja kufuatia changamoto ambayo dunia inaendelea kuipitia ya UVIKO 19, na nyuki wamesaidia kwenye mapambani dhidi ya janga hili kwa kuimarisha kinga za miili ya watu.

Pamoja na uwepo wa kaulimbiu hiyo ya kidunia, kaulimbiu ya kitaifa kwa mwaka huu wa 2022, nayo inasema “NYUKI NI UCHUMI: TUWALINDE NA KUHIFADHI MAZINGIRA YAO”. Kaulimbiu hii inaendana na ile ya kidunia kwa kuendelea kuhamasisha wadau kuendelea kutambua umuhimu wa kuwalinda na kuwahifadhi nyuki ili kupata manufaa ya kiuchumi na kiafya.

WAKE WAWILI WA WAZIRI AWESO WALIVYOIBUA SHANGWE BUNGENI MWENYEWE ASEMA “NAWAPENDA SANA”

You Might Also Like

Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mayanja atoa maagizo haya kwa Wakulima Wilayani humo

Picha: Polisi Jamii Cup yazinduliwa Mkoani Manyara

Mkurugenzi wa Asas afunguka, ‘Tunawafugaji Elfu 6500, Rungwe na Isanu Busokelo uzalishaji ni mkubwa’

Mfanyabiashara maarufu Marcas ajitosa kuutaka U NEC Arusha, kufuatia kufutwa kwa Uchaguzi mwaka jana

Wananchi Wilayani Korogwe wamuomba hili DC Jokate kutafuta ufumbuzi, ‘Changamoto ya Tembo’

Edwin TZA May 12, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Mwijaku aonesha kufuru ya Harmonize, gari jipya lenye jina la Kajala latua Dar
Next Article A$AP Rocky katuletea hii video mpya ya wimbo wake, Rihanna aonekana (video+)
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 26, 2023
Magazeti March 26, 2023
Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mayanja atoa maagizo haya kwa Wakulima Wilayani humo
Top Stories March 25, 2023
Gigy Money katuletea hii video mpya ‘ogopa’ itazame hapa
Entertainment March 25, 2023
Picha: Polisi Jamii Cup yazinduliwa Mkoani Manyara
Top Stories March 25, 2023

You Might also Like

Top Stories

Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mayanja atoa maagizo haya kwa Wakulima Wilayani humo

March 25, 2023
Top Stories

Mkurugenzi wa Asas afunguka, ‘Tunawafugaji Elfu 6500, Rungwe na Isanu Busokelo uzalishaji ni mkubwa’

March 25, 2023
Top Stories

Mfanyabiashara maarufu Marcas ajitosa kuutaka U NEC Arusha, kufuatia kufutwa kwa Uchaguzi mwaka jana

March 25, 2023
Top Stories

Wananchi Wilayani Korogwe wamuomba hili DC Jokate kutafuta ufumbuzi, ‘Changamoto ya Tembo’

March 25, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?