Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Madiwani Ngorongoro waigomea Rasimu ya mpango wa matumizi ya ardhi “Madiwani hawajui kiingereza”
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa Magazetini Kenya leo June 4, 2023
June 4, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 4, 2023
June 4, 2023
Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia
June 3, 2023
Mapokezi ya ndege ya kwanza ya mizigo aina ya Boeing 767 -300F
June 3, 2023
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuapishwa kuliongoza taifa hilo
June 3, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Madiwani Ngorongoro waigomea Rasimu ya mpango wa matumizi ya ardhi “Madiwani hawajui kiingereza”
Top Stories

Madiwani Ngorongoro waigomea Rasimu ya mpango wa matumizi ya ardhi “Madiwani hawajui kiingereza”

May 25, 2023
Share
4 Min Read
SHARE

Madiwani wa Baraza la Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro Mkoa wa Arusha,wameikataa rasimu ya mpango wa matumizi ya Ardhi ya wilaya hiyo, wakidai si shirikishi na inalenga kumega ardhi yao ya malisho na kuiingiza kwenye hifadhi kitendo ambacho wamedai kitaathiri ustawi wa Wananchi .

Madiwani hao walitoa kauli hiyo katika baraza hilo la madiwani baada ya kuwasilishwa kwa ajenda namba nne katika kikao hicho iliyolenga kujadili na kupitisha mpango wa matumizi ya Ardhi wa miaka 20 kuanzia mwaka huu 2023 hadi 2043.

Diwani wa kata ya Nainokanoka,Edward Maura alisema hawakubaliani na rasimu hiyo kwa kuwa imelenga kuchukua sehemu kubwa ya Ardhi yao na kuifanya sehemu ya eneo la hifadhi jambo litakaloathiri ustawi wa maisha yao na malisho ya mifugo.

Maura ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la wafugaji alifafanua kuwa ,wilaya ya Ngorongoro inakata 28,vijiji 72 ikiwa na ukubwa wa Ardhi ya kilometa za mraba 14,030 na asilimia 75 ni hifadhi na asilimia 25 ni matumizi ya wananchi ikiwemo malisho ,hivyo kupitisha rasimu hiyo ni kuhatarisha makazi ya wananchi wapatao 274,000.

“Sisi kama madiwani tumeweka saini zetu kwa pamoja kukataa rasimu hiyo na sababu za kukataa ni pamoja na serikali kuchukua eneo letu kubwa na kubakiwa na asilimia 25 tu”alisema

Aliongeza kuwa mpango wa matumizi ya Ardhi wa wilaya ya Ngorongoro haukufuata matakwa ya sheria ya kushirikisha mikutano mikuu halali ya vijiji ,hivyo kupitisha mpango huo ni kuhalalisha mwisho wa kuishi kwa kuendelea kukosa makazi,kilimo na nyanda za malisho.

Naye diwani wa viti maalumu kata ya Kakesio, tarafa ya Ngorongoro ,Sein Lekeni alisema sababu ya kukataa rasimu hiyo ni kutoshirikishwa kwa wananchi na kupewa elimu juu ya umuhimu wa jambo hilo na iwapo tutaikubali tutakuwa watu wa ajabu sana .

 

“Leo tulikuwa kwenye kikao cha baraza la madiwani , tumekataa ile rasimu iliyokuwa imeletwa kwenye baraza kwa sababu sio shirikishi ni rasimu ambayo imepangwa na watu fulani ,na tukipitisha tutakuwa madiwani wa ajabu sana ,sisi sote madiwani 32 tumeikataa kwa kuweka saini zetu ”

Diwani mwingine ,James Moringe wa kata ya Laitore,alisema ajenda ya matumizi ya ardhi ya miaka 20 katika wilaya ya Ngorongoro haina tija na wameikataa kwa sababu imetenga wilaya hiyo kijiografia .

 

Alisema utaratibu kama huo uliwahi kutumiwa na serikali kupima eneo lao la malisho lenye ukubwa wa kilometa za mraba 1500 na kulifanya pori tengefu kinyume cha sheria ,suala waliosisitiza kuwa hawakubaliani na rasimu hiyo.

“Hakuna mikutano ya wananchi iliyotumika kuzungumzia suala hilo kuanzia tarafa ya Ngorongoro ambako ndio yaliko makazi ya wamasai”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza hilo la Madiwani,Mohamed Bayo alisema kuwa raimu hiyo haikuweza kupita kwa sababu iliandikwa kwa Lugha ya Kiingereza na madiwani wa jamii ya wafugaji wengi wao hawajui kiingereza hivyo niliamuru ikafanyiwe marekebisho.

Hata hivyo mwenyekiti huyo alisema anakubaliana na ras
imu hiyo ila alisema lazima ifanyiwe marekebisho kwani hakuna serikali inayochukia wananchi wake na anaimani mpango wa serikali ni mzuri .

You Might Also Like

Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia

Mapokezi ya ndege ya kwanza ya mizigo aina ya Boeing 767 -300F

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuapishwa kuliongoza taifa hilo

Watu 288 sasa wamethibitishwa kufarikiwengine 900 kujeruhiwa katika ajali ya treni India

Ukraine iko tayari kuzindua mashambulizi-Volodymyr Zelensky

Edwin TZA May 25, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Shule ya Ibun Jazar wakomalia maadili mema kwa Viongozi wajao
Next Article Fei toto hajakubali yaishe, aomba mchango kwa Watanzania, kufungua kesi ‘CAS’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa Magazetini Kenya leo June 4, 2023
Magazeti June 4, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 4, 2023
Magazeti June 4, 2023
Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia
Top Stories June 3, 2023
Mapokezi ya ndege ya kwanza ya mizigo aina ya Boeing 767 -300F
Top Stories June 3, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia

June 3, 2023
Top Stories

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuapishwa kuliongoza taifa hilo

June 3, 2023
Top Stories

Watu 288 sasa wamethibitishwa kufarikiwengine 900 kujeruhiwa katika ajali ya treni India

June 3, 2023
Top Stories

Ukraine iko tayari kuzindua mashambulizi-Volodymyr Zelensky

June 3, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?