Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Majibu ya Serikali kuhusu dhamana kwa makosa ya uhujumu uchumi
Share
Notification Show More
Latest News
Waziri Dr Damas Ndumbaro na Rais TFF watinga AVIC Town kuzungumza na wachezaji wa Yanga SC
September 29, 2023
Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu
September 29, 2023
Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA
September 29, 2023
Mohbad: Polisi wa Lagos wamkamata Sam Larry ahusishwa na kifo cha Mohbad
September 29, 2023
Reece James kurejea kikosoini hivi karibuni- Chelsea
September 29, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Majibu ya Serikali kuhusu dhamana kwa makosa ya uhujumu uchumi
Top Stories

Majibu ya Serikali kuhusu dhamana kwa makosa ya uhujumu uchumi

January 31, 2020
Share
3 Min Read
SHARE

Serikali imesema kuwa endapo Mbunge ataona kuwa kuna haja ya kubadilishwa Sheria ya makosa ya uhujumu uchumi ili watuhumiwa wa makosa hayo yawe na dhamana awasilishe hoja yake Bungeni kwani Bunge ndiyo chombo chenye mamlaka ya kutunga na kubadili sheria.

Hayo yamesemwa Bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandishi Hamad Masauni wakati wa kipindi cha maswali na majibu katika kikao cha pili cha mkutano wa 18 wa Bunge la 11 alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum, Sabreena Hamza Sungura.

Katika swali lake Mbunge huyo aliuliza, “Kutokana na msongamano wa mahabusu na wafungwa magerezani, Je! Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa kubadili sheria hiyo ili Majaji waweze kutoa dhamana kwa watuhumiwa, kwani kwa hali ilivyo sasa hata mtu anayetuhumiwa kuhujumu Tsh 20,000 ananyimwa dhamana?

“Ni mamlaka ya Bunge hili kutunga sheria na kubadilisha pale unapoona inafaa, na yeye ni mbunge wa Bunge hili na kanuni anazifahamu. Kama anaona kuna utaratibu unaofaa (kubadili sheria), ni haki ya mbunge kutumia haki yake ya kikanuni,” amejibu Masauni.

Wakati huo huo, Mbunge wa Vunjo, James Mbatia amehoji kwanini Serikali haifuati utaratibu ulioelezwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma ambapo alitaka upelelezi wa kesi kukamilika kwanza kabla ya mtuhumiwa kukamatwa.

Mbatia ameongeza kuwa kuna haja ya sheria hiyo kubadilishwa ieleze kuwa mtu akishikiliwa kwa miezi mitatu na upelelezi usipokamilika basi aachiwe huru.

Akijibu maswali hayo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema wakati watu wakiendelea kushabikia mambo haya ni kweli anatambua kwamba watuhumiwa na wafungwa wana haki, lakini pia wale waliotendewa makosa pia wana haki, hivyo watu wasiangalie upande mmoja tu.

“Ziko haki za wafungwa, ziko haki za watuhumiwa, lakini ziko pia haki za waliotendewa makosa. Kwa hiyo tusilichukulie jambo hili kama ni jepesi jepesi, lazima lichujwe, liangaliwe, na uko utaratibu wa kisheria wa kufanya mambo haya. Tusikimbilie tu kushabikia haki za hawa waliotenda makosa, lakini ziko pia za waliotendewa makosa,” amebainisha Simbachawene.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania kwa sasa, mtu akishtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi, mahakama haina mamlaka ya kumpa dhamana, na kwamba atakaa rumande hadi hapo hukumu ya kesi itakapotolewa ama aachiwe huru au apewe adhabu.

BREAKING: MAGUFULI AMTUMBUA LUGOLA “UNANITESA, ONDOKA HAPA SINA URAFIKI KAZINI”

You Might Also Like

Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA

Mohbad: Polisi wa Lagos wamkamata Sam Larry ahusishwa na kifo cha Mohbad

Reece James kurejea kikosoini hivi karibuni- Chelsea

Rais wa Urusi Vladimir Putin akutana na kamanda mkuu wa zamani wa Wagner Group

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA January 31, 2020
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Lugola awasili TAKUKURU na Ilani ya CCM mkononi
Next Article “Serikali haitawavumilia Watendaji wa Vyama vya Ushirika” Kamani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Waziri Dr Damas Ndumbaro na Rais TFF watinga AVIC Town kuzungumza na wachezaji wa Yanga SC
Sports September 29, 2023
Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu
Top Stories September 29, 2023
Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA
Top Stories September 29, 2023
Mohbad: Polisi wa Lagos wamkamata Sam Larry ahusishwa na kifo cha Mohbad
Entertainment September 29, 2023

You Might also Like

Top Stories

Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

September 29, 2023
Top Stories

Ufanisi wa wataalamu waipaisha TBA

September 29, 2023
Sports

Reece James kurejea kikosoini hivi karibuni- Chelsea

September 29, 2023
Top Stories

Rais wa Urusi Vladimir Putin akutana na kamanda mkuu wa zamani wa Wagner Group

September 29, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?