Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Maoni ya Ezekiel Kamwaga kuhusu uteuzi wa January Makamba
Share
Notification Show More
Latest News
MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
March 24, 2023
Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’
March 24, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Maoni ya Ezekiel Kamwaga kuhusu uteuzi wa January Makamba
Top Stories

Maoni ya Ezekiel Kamwaga kuhusu uteuzi wa January Makamba

September 28, 2021
Share
3 Min Read
SHARE

Imeandikwa na Kaimu Afisa Habari wa Simba SC Ezekiel Kamwaga

TANESCO ni shirika la huduma lakini pia ni shirika la kibiashara ndio maana kila mwaka linakaguliwa mahesabu na ripoti ya hasara au faida inatolewa kwa umma.

Kama halistahili kuendeshwa kibiashara kungekuwa hakuna haja ya kila mwaka kuripoti faida au hasara, na kungekuwa hakuna haja ya kutakiwa kutoa gawio serikalini.

Shirika linalotakiwa kupata faida ni lazima liendeshwe kwa misingi ya kibiashara – ikiwemo kuongeza tija, kupunguza matumizi, kuongeza mauzo, kuwajali wateja kwa kuwapa huduma bora, kuajiri wafanyakazi kwa sifa na kuwajali kwa maslahi stahiki, kuongeza rasilimali zake, na mambo mengineyo ambayo kampuni zenye mafanikio hupaswa kufanya.

Ni dhana potofu kuamini kwamba Shirika la Umma halipaswi kuzingatia misingi hii ya kibiashara. Ni upotofu pia kuamini kwamba Shirika la Umma likizingatia misingi hii basi gharama za huduma zinapanda. Ukweli ni kinyume.

Hakuna kundi la Watanzania – wawe wasomi, makada wa vyama vya siasa au watumishi wa serikali kuwa pekee ndio wenye uwezo, maarifa na uzalendo kwenye usimamizi wa mali za umma. Kama huo ndiyo ungekuwa ukweli, nchi yetu isingefika hapa ilipo sasa ambapo tunatumia fedha za kununulia dawa na madawati kuruzuku mashirika ya umma.

China imekuwa na mashirika mengi makubwa ya umma. Kwenye wimbi la ubinafsishaji, China ikasita kubinafsisha. Ilichofanya ni kuamua kuyaendesha kibiashara.

Sasa hivi sehemu kubwa ya uchumi wa China inaendeshwa na mashirika yao ya umma. Ilifanya hivyo kwa kuwapa uendeshaji wa mashirika yake watu wenye uzoefu wa kuendesha biashara.

Ufaransa ina mashirika ya umma ambayo hata Wakurugenzi watendaji wake si Wafaransa. Wametafuta watu kote duniani wenye uwezo na kuwapa kazi kuyaendesha mashirika yao kibiashara kwa faida ya Wafaransa wote.

Hapa kwetu uteuzi wa Bodi mpya ya Tanesco iliyojaa Watanzania (ambao hawajahukumiwa kwa kosa lolote) imeonekana kama si jambo la heri katika macho na nafsi za baadhi ya watu wachache.

Huko kwa wenzetu waliofanikiwa mashirika makubwa ya umma ya umeme yanauza sehemu ya hisa zake kwenye masoko ya mitaji.

Mheshimiwa Makamba ameonyesha ujasiri na kutoa dira ya namna ambavyo mashirika yetu yanapaswa kuendeshwa.

Unatafuta best brains kwenye nchi na unawapa. Kama mmiliki (yaani Serikali) unatoa malengo ya jumla: kwamba unataka huduma bora, huduma kila pahala na huduma nafuu na unataka gawio pia.

Mwalimu Nyerere alipata kusema huko nyuma kwamba kufanya mambo kwa namna ileile na kutegemea kupata matokeo tofauti ni jambo lisilo la akili.

Waziri Makamba amejaribu kufanya kitu tofauti. Tusubiri kuona kama tutapata tunachohitaji kutoka Tanesco.

Bahati nzuri ni kwamba njia aliyoamua kuipitia, ndiyo njia ambayo imefanikiwa kwa wenzetu.

MAKAMBA ATINGA TANESCO ATOA MAAGIZO MAZITO “TUTAWAONDOA KATIKA NAFASI ZENU”

You Might Also Like

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

TAGGED: January Makamba
Edwin TZA September 28, 2021
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Maajabu ya mtu anaetumia mapafu ya chuma, shingoni hadi miguuni kumepooza (video+)
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 29, 2021
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
Top Stories March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
Top Stories March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
Top Stories March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
Top Stories March 24, 2023

You Might also Like

Top Stories

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

March 24, 2023
Top Stories

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

March 24, 2023
Top Stories

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

March 24, 2023
Top Stories

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

March 24, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?