Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Mchimba madini akamatwa kwa mauaji
Share
Notification Show More
Latest News
Jorginho aondoka Chelsea na kusaini Arsenal
February 1, 2023
Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain
January 31, 2023
Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza
January 31, 2023
Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)
January 31, 2023
Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg
January 31, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Mchimba madini akamatwa kwa mauaji
Top Stories

Mchimba madini akamatwa kwa mauaji

November 28, 2022
Share
2 Min Read
SHARE

JESHI la Polisi mkoani Mbeya limemkamata mchimbaji na mnunuzi wa madini, Ezekiel Luhwesha (31) akituhumiwa kumuua wakala wa maegesho ya magari jijini Mbeya, William Mgaya (58).

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga alisema Luhwesha ambaye ni mkazi wa wilayani Chunya mkoani Mbeya, anatuhumiwa kumuua Mgaya Novemba 26 saa 4:30 asubuhi katika eneo la Mafiati kata ya Ruanda kwenye ofisi za Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (Tarura) jijini humo.

Kamanda Kuzaga alisema jana kuwa siku ya tukio, Mgaya na mwezake Almasi Shaban (32) wote wakala wa maegesho ya magari,wakiwa katika kazi yao ya kukusanya ushuru walimkamata Ezekiel baada ya kuscan namba ya gari lake T 772 DVY Toyota Hilux.

Ilidaiwa kuwa gari lilikuwa likidaiwa Sh 7,500 na mtuhumiwa alitakiwa kulipa deni hilo lakini alihitaji kuhakiki deni hilo hivyo waliongozana hadi ofisi za Tarura.

“Baada ya kuoneshwa taarifa katika mfumo, mtuhumiwa aliliridhika na kuahidi kulipa deni hilo,lakini wakala Willium Mgaya alimtaka kulipa deni hilo papo kwa hapo kwa sababu deni hilo ni la muda mrefu na ndipo yalitokea majibizano yasiyo rafiki kati yao na kupelekea mtuhumiwa kutoa pisto yake na kumfyatulia risasi kifuani Willium Mgaya na kupoteza maisha muda mfupi baada ya kufikishwa hospitali ya rufaa Mbeya kwa matibabu,”alisema Kamanda Kuzaga.

Alisema mtuhumiwa yupo polisi na silaha yake aina ya bastola yenye namba T.0620-19J0037 ikiwa na risasi tisa ndani ya magazini inashikiliwa.

Kamanda Kuzaga alihimiza wamiliki wa silaha za moto wazingatie masharti ya umilikishwaji kama walivyoomba na wasizitumie tofauti na masharti yalivyoeleza ikiwa ni pamoja kujichukulia sheria mkononi.

You Might Also Like

Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain

Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza

Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)

Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg

Biden akataa kutuma ndege za kivita Ukraine

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA November 28, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Ahukumiwa kuchapwa viboko 24
Next Article Tanzania yang’ara mashindano ya kuogelea ya kanda ya tatu Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Jorginho aondoka Chelsea na kusaini Arsenal
Sports February 1, 2023
Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain
Top Stories January 31, 2023
Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza
Top Stories January 31, 2023
Waliokutwa na meno ya tembo wahukumiwa miaka 20 jela (+video)
Top Stories January 31, 2023

You Might also Like

Top Stories

Rais Samia ashtukia mchezo mchafu hela za Plea Bargain

January 31, 2023
Top Stories

Rais Samia ainyooshea kidole Polisi, Magereza

January 31, 2023
Top Stories

Maji ya ajabu yanayotoka bombani Johannesburg

January 31, 2023
Top Stories

Biden akataa kutuma ndege za kivita Ukraine

January 31, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?