Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Rais Magufuli Ikulu akutana na Dr. Bashiru na Viongozi wa AALCO (+video)
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa Magazetini Kenya leo May 30, 2023
May 30, 2023
Katibu Mkuu CCM amuagiza haya RC wa Iringa, kuhakikisha kituo hiki cha Afya kimefunguliwa na kuanza kutoa huduma
May 30, 2023
GSM Home wametuonesha bidhaa za ndani walizopunguza mpaka asilimia 60%, wahi sasa
May 30, 2023
Katibu wa NEC anena kuhusu mfumo wa M-Mama, utasaidia kupunguza vifo vya akina Mama Wajawazito
May 30, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo May 30, 2023
May 30, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Rais Magufuli Ikulu akutana na Dr. Bashiru na Viongozi wa AALCO (+video)
Top Stories

Rais Magufuli Ikulu akutana na Dr. Bashiru na Viongozi wa AALCO (+video)

October 23, 2019
Share
3 Min Read
SHARE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na viongozi wa Taasisi ya Mashauriano ya Kisheria kwa Nchi za Asia na Afrika (AALCO) ambao wanahudhuria mkutano wa 58 unaofanyika hapa nchini kwa siku 5 ukiwakutanisha wajumbe kutoka nchi wanachama 49 na mashirika mbalimbali.

Viongozi wa AALCO waliokutana na Rais Magufuli ni Rais wa AALCO, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Waziri wa Sheria na Katiba, Tanzania), Makamu wa Rais wa AALCO Prof. Mohamad Shalaldeh (Waziri wa Sheria wa Palestina), Katibu Mkuu wa AALCO Prof. Kennedy Gastorn (Tanzania) na Naibu Makatibu Wakuu wa AALCO watatu ambao ni Yukihiro Takeya (Japan), Wang Liyu (China) na Dr. Ali Garshasbi (Iran).

Rais Magufuli amewashukuru na kuwakaribisha wajumbe wa AALCO nchini Tanzania na amewahakikishia kuwa Serikali inatambua kazi inayofanywa na taasisi hiyo tangu ijiunge nayo mwaka 1965 na kuwa mwanachama kamili kuanzia mwaka 1973.

Rais Magufuli amesisitiza umuhimu wa AALCO kutekeleza malengo ya taasisi hiyo kama alivyoelezwa na viongozi hao, na ametoa wito wa kuendelea kuzitetea nchi wanachama hasa zinazowekewa vikwazo mbalimbali.

Ametolea mfano wa Zimbabwe ambayo imewekewa vikwazo kwa miaka mingi hali inayosababisha wananchi wa Zimbabwe kuteseka.

Rais wa AALCO Balozi Mahiga na Katibu Mkuu Prof. Kennedy Gastorn wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kupata fursa ya kukutana nae na wameahidi kuwa AALCO itaendelea kutekeleza majukumu yake kwa maslahi ya Asia na Afrika.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba Mhe. Amon Mpanju.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Ndg. Guo Yezhou, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amemuomba Yezhou kufikisha shukrani zake kwa Rais wa China na Mwenyekiti wa CPC Mhe. Xi Jinping kwa kutoa tuzo kwa Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuiwezesha China kuwa mwanachama wa Umoja wa Mataifa.

Rais Magufuli amemhakikishia kuwa Sera za Tanzania kuhusu China hazijabadilika na amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na China katika jitihada mbalimbali za maendeleo.

Mazungumzo hayo yamehudhriwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bashiru Ally Kakurwa na Balozi wa China hapa nchini Wang Ke.

IKULU LEO “VIKWAZO SI HALALI, VIONDOLEWE HARAKA IWEZEKANAVYO”

You Might Also Like

Katibu Mkuu CCM amuagiza haya RC wa Iringa, kuhakikisha kituo hiki cha Afya kimefunguliwa na kuanza kutoa huduma

GSM Home wametuonesha bidhaa za ndani walizopunguza mpaka asilimia 60%, wahi sasa

Katibu wa NEC anena kuhusu mfumo wa M-Mama, utasaidia kupunguza vifo vya akina Mama Wajawazito

Waziri Masauni asimama Bungeni Mei 29, 2023 ‘Watanzania 66 waukana Uraia’

Sentensi za Mkurugenzi wa Asas kwenye Mkutano Mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT)

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA October 23, 2019
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Rais Magufuli afanya uteuzi Ikulu leo
Next Article IKULU LEO “Vikwazo si halali, viondolewe haraka iwezekanavyo” (+video)
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa Magazetini Kenya leo May 30, 2023
Magazeti May 30, 2023
Katibu Mkuu CCM amuagiza haya RC wa Iringa, kuhakikisha kituo hiki cha Afya kimefunguliwa na kuanza kutoa huduma
Top Stories May 30, 2023
GSM Home wametuonesha bidhaa za ndani walizopunguza mpaka asilimia 60%, wahi sasa
Top Stories May 30, 2023
Katibu wa NEC anena kuhusu mfumo wa M-Mama, utasaidia kupunguza vifo vya akina Mama Wajawazito
Top Stories May 30, 2023

You Might also Like

Top Stories

Katibu Mkuu CCM amuagiza haya RC wa Iringa, kuhakikisha kituo hiki cha Afya kimefunguliwa na kuanza kutoa huduma

May 30, 2023
Top Stories

GSM Home wametuonesha bidhaa za ndani walizopunguza mpaka asilimia 60%, wahi sasa

May 30, 2023
Top Stories

Waziri Masauni asimama Bungeni Mei 29, 2023 ‘Watanzania 66 waukana Uraia’

May 29, 2023
Top Stories

Sentensi za Mkurugenzi wa Asas kwenye Mkutano Mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT)

May 29, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?