Mashindano ya Miss Higher Learning yamerudi tena 2023 baada ya awali 2022 kutofanyika, mashindano hayo yanatarajia kufanyika March 2023.
Kwa upande wa usaili utafanyika February 11 2023 Hug Mug Cafe Masaki jijini Dar es Salaam na vigezo vya ushiriki ni kuanzia warembo wa vyuo Vikuu wenye miaka 18-24.
Kuelekea kuanza kwa usaili wa mashindano hayo wakati wa uzinduzi Miss Higher Learning 2021/22 Otaigo Mwema alikuwepo na ametoa neno kwa warembo wenye nia ya kushiriki na faida ya mashindano hayo.
“Mwaka 2021 nilivyokuja kwenye usaili nilikuwa msichana mdogo naogopa vitu vingi sana kushindwa naogopa kushindana naogopa kujitoa kuonesha kipaji nilicho nacho lakini kitu ambacho nilikuwa na uhakika nacho ni ule moyo wa kuthubutu”>>> Otaigo Mwema
“Mara nyingi vijana wadogo hawajui pakuanzia ni wapi lakini namshukuru Mungu Miss Higher Learning imekuwa ni moja ya mlango uliyofunguka mimi niweze kuwaza ndoto zangu”>>> Otaigo
Otaigo ambaye ni Miss Higher Learning 2021 pia alikuwa mshindi namba 3 wa Miss Tanzania 2022 lakini pia ndio muwakilishi wa Tanzania kwenye mashindano ya Miss University Afrika 2023 ambapo tarehe itatangazwa hapo baadae.