Kampuni ya Premier Bet Tanzania imemtambulisha mshindi wa kubashiri soka ambaye ni Andrea Sebastian mkazi wa Igunga, Tabora ambaye ameshinda zaidi ya Mil.50.
Uongozi wa Kampuni hiyo umenpongeza Sebastian na kumkabidhi hundi ya Sh.Mil 53,636,841 katika Makao Makuu ya Ofisi za Primier Bet.
Akizungumzia ushindi huo, Sebastian mwenye miaka (23) amesema hakutarajia kupata kiasi hicho cha Mil.50 kwa sababu alitumia Sh.1000 kucheza.
Meneja Masoko wa Primier Bet, Erick Kirita amesema wanampongeza Sebastian kwa ushindi huo, huku akitoa wito kwamba kubashiri ni mchezo wa kujifurahisha na sio chanzo cha mapato.
“Kima cha chini cha ubashiri ni Sh.200 mtandaoni na 500 katika maduka ya mawakala, kiwango cha juu cha ushindi ni Milioni 238,”amesema.
MZEE AMUUMBUA ‘HAKIMU’ MBELE YA WAZIRI “ALIPEWA LAKI TANO NA MOLLEL”