Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Morocco Square yawapa wazimu NHC kujenga miradi
Share
Notification Show More
Latest News
MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
March 24, 2023
Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’
March 24, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Morocco Square yawapa wazimu NHC kujenga miradi
Top Stories

Morocco Square yawapa wazimu NHC kujenga miradi

January 27, 2023
Share
4 Min Read
SHARE

Shihirika la nyumba Tanzania (NHC) limeingia mkataba na kampuni ya KingJada Hotel and Apartment katika eneo la Morocco Square jijini Dar es salaam kwa ajili ya huduma za hotel ya kisasa ambayo itakuwa inahudumia watu wengi kuliko hotel zote katika jijini hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Nyumba Tanzania NHC Nehemia Mchechu amesema kuwa wamesaini mkataba wa uwekezaji wa HOTELI ya KingJada Hotel and Apartments Ltd Katika eneo la Morocco Square jijini Dar es salaam leo Ijumaa 27,2023 kwa mkataba wenye manufaa ya wateja wengi watakaoishi na kupata huduma katika eneo hilo muhimu.

Utiaji saini wa mkataba huu wa upangaji wa hotel ya Mradi wa Morocco Square kati ya NHC na KingJada Hotels & Apartments Ltd ni ishara ya uthubutu na imani ya sekta binafsi kwa Shirika na nchi kwa ujumla. KingJada Hotel & Apartments ni mmojawapo kati ya wawekezaji kadhaa ambao waliomba nafasi ya kuendesha hotel hii na ambaye amekidhi vigezo tulivoweka, ambavyo ni kupanga na hatimaye kununua hoteli. Mwekezaji huyu amepatikana miongoni wa wawekezaji wengi waliowasilisha mapendekezo yao ya biashara.

Nataka nimhakikishie mwekezaji huyu kuwa tutampa ushirikiano wa kutosha ili aweze kutimiza malengo yake na yetu tuliyojiwekea kwani sisi kama Shirika tunamkabidhi jengo la kisasa likiwa na huduma zote muhimu ukiwamo umeme wa uhakika, miundombinu ya zimamoto, mfumo wa vipoza joto, miundombinu ya mtandao wa mawasiliano, lifti, ulinzi wa saa 24 wa kamera za CCTV na kisima kirefu cha maji chenye mfumo wa kusukuma maji ya kutosha.

“Kwangu ni furaha kubwa siku ya leo kwa sababu inatufanya tuanze kufunga zile hatua muhimu za uwekezaji wetu ili watu waanze kutumia hizi huduma, Ingekuwa ni Kichaa ningesema NHC tumepata wazimu wa kujenga na kujenga miradi zaidi, Lakini Wazimu mzuri na wa maendeleo hii inatokana na kwamba tunayo miradi mingi ambayo tutaendeleza kuijenga karibu nchi nzima ili kuleta maendeleo katika uwekezaji wa sekta ya nyumba nchini,” Amesema Nehemia Mchechu

Mchechu ameongeza kuwa anatamani hoteli hiyo ifunguliwe wakati wa sikukuu za pasaka au Idd kwa sababu  itakuwa na uwezo wa kupokea wateja wengi kuliko hotel zote jijini Dar es salaam ukizingatia kwamba eneo la Morocco Square litaweza kutembelewa na watu elfu 10.000 kwa siku moja jambo ambalo linaiweka hoteli ya KingJada kuwa katika uwezo mzuri wa kufanya biashara mara itakapoanza kazi

Mchechu ametanabaisha kuwa mojawapo ya sehemu muhimu ya mradi huo ni jengo hili linalotoa huduma za hoteli. Sehemu hii ni muhimu sana kwa sababu ndiyo inayokamilisha dhana nzima ya mradi huu ya kuishi, kufanya kazi, kununua bidhaa na kupata mapumziko mahala pamoja (live, work, shop and enjoy at the same location).

Amesema kusainiwa kwa mkataba wa upangaji na uendeshaji wa hoteli hii leo ni ishara ya kuwa katika hatua za mwisho za umaliziaji wa ujenzi na hatua za mwanzo za ufunguzi wa mradi. Hatua hii inatoa ishara kubwa na muhimu sana katika sekta ya miliki kwa kukamilisha mojawapo ya miradi mikubwa sana ya ujenzi Nchini Tanzania.

Mchechu amewashukuru wadau mbalimbali wanaoshirikiana nao katika mradi huo ambao ni Hotel & Apartments, Mkandarasi wa mradi huu (Estim Construction), wanunuzi wa nyumba na ofisi za mradi huu, wapangaji wa maeneo ya biashara ya mradi huu, wabia wa taasisi za fedha, na timu ya NHC kwa jitihada zenu zote na kazi ya kitaalamu kuwezesha hafla hii ya utiaji saini ikafanikiwa.

You Might Also Like

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

Pascal Mwakyoma TZA January 27, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Picha: Mwili wa Mtanzania aliefia kwenye vitani urusi, waagwa kwa picha nyumbani kwao
Next Article Mkali Lord Eyez ametuletea hii collabo yake akiwa na Adiana Ross
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
Top Stories March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
Top Stories March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
Top Stories March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
Top Stories March 24, 2023

You Might also Like

Top Stories

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

March 24, 2023
Top Stories

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

March 24, 2023
Top Stories

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

March 24, 2023
Top Stories

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

March 24, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?