Rais wa Klabu ya Yanga na Mwenyekiti wa Vilabu Barani Afrika, Eng Hersi Said @caamil_88 amekutana na Rais wa Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) @psg ya Ufaransa na Mwenyekiti wa Vilabu Barani Ulaya, Ndugu Nasser Bin Ghanim Al-Khelaifi, Jijini Paris Nchini Ufaransa, jana Januari 3, 2023.
Eng Hersi alipewa mualiko maalum kutoka Kwa ndugu Nasser Bin Ghanim Al-Khelaifi kwa lengo la kujadili jinsi vyama hivyo vikubwa vinavyoweza kujenga uhusiano mzuri utakaosaidia maendeleo ya Vilabu Wanachama.
Vilevile, Ndugu Nasser Bin Ghanim Al- Khelaifi alimkaribisha Eng Hersi kushuhudia mchezo wa Fainali ya Trophée des Champions uliochezwa kwenye Uwanja wa Parc de Prince, ambapo PSG ilibeba Ubingwa baada ya kuichapa Toulouse kwa magoli 2-0.
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_415008804_18304676224135476_6770626283810952291_n_1080-1-761x950.jpg)
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_414999913_18304676215135476_3380680826035882225_n_1080-760x950.jpg)
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_414990949_18304676206135476_6219008797419090736_n_1080-760x950.jpg)
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_414979251_18304676194135476_6030457768726054892_n_1080-760x950.jpg)
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_414976257_18304676185135476_2588329047385086368_n_1080-760x950.jpg)
![](https://millardayo.com/wp-content/uploads/2024/01/Snapinsta.app_414997303_18304676176135476_4395050075711973619_n_1080-760x950.jpg)