Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Picha za ajali iliyoua wanafunzi watano Mtwara leo Jan 22 pamoja na taarifa kamili.
Share
Notification Show More
Latest News
Watumishi watakiwa kujipanga kustaafu pindi wanapoajiriw.
September 30, 2023
Anthony kurejea mazoezini baada ya sekeseke lililomkuta.
September 30, 2023
TASAC kusisitiza matumizi sahihi ya vyombo vya majini.
September 30, 2023
Maboresho ya bandari kusaidia ufanisi katika kazi.
September 30, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 30, 2023
September 30, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Mix > Picha za ajali iliyoua wanafunzi watano Mtwara leo Jan 22 pamoja na taarifa kamili.
Mix

Picha za ajali iliyoua wanafunzi watano Mtwara leo Jan 22 pamoja na taarifa kamili.

January 22, 2014
Share
2 Min Read
SHARE
IMG-20140122-WA0006Wanafunzi watano wa shule ya sekondari Mustafa Sabodo iliyopo nje kidogo ya mji wa Mtwara wamefariki Dunia na wengine 47 kujeruhiwa baada ya kugongwa na gari wakati  wakikimbia mchakamchaka mapema leo asubuhi.

Taarifa inasema kuwa gari hilo lenye namba za usajili T174 AED aina ya Mercides Benz lilikuwa likiendeshwa na Dereva Baraka Mgwegwe ambapo likiwa kwenye mwendo kasi liliacha njia na kuwagonga wanafunzi hao ambao walikuwa kandokando ya barabara wakikimbia mchakamchaka kurejea shuleni.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara Zelothe Steven na Mganga Mkuu wa hospital hiyo wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na amewataja wanafunzi waliopoteza maisha kwa ajali hiyo ni pamoja na Khairati Mohamed Said, Mwanahamisi Mohamed,Nasma Salum Mpunja, Hilda Matias Nguli na Farida Ally ambao wote wanasoma kidato cha kwanza katika shule hiyo.
Mpaka sasa hali za majeruhi 21  waliolazwa hospitalini hapo zinaendelea vizuri ukiondoa mmoja ambaye amehamishiwa katika hospitali ya mission Nyangao mkoani Lindi kwa matibabu Zaidi huku dereva aliyesababisha ajali hiyo akishikiliwa na polisi kusubiri sheria kufuata mkondo wake.
Dereva Baraka Mgwegwe ameongea na millardayo.com na kusema>>’Nimetoka nyumbani kwangu sa 10 na nusu alfajiri naelekea kumpeleka Mgonjwa Lindi  Hospital nilikuwa na ndugu zangu wawili na mgonjwa kwenye gari,tulipofika maeneo ya Pacha ya kwenda Mchuchu mbele yangu kulikua na lori imesimama na nyuma ya lori ndio kunasadikiwa kuwa kulikuwa na hao wanafunzi’
‘Mimi nilikuwa nimejiandaa kupishana na hiyo lori na wanafunzi nao wanaingia barabarani sehemu ambayo mimi nilikuwa najiandaa kupita mimi sikumuona mwanafunzi hata mmoja kilichotokea pale nikutokea kwa hiyo ajali ya kuwagonga hao wanafunzi baada ya kuwagonga nikaenda kusimama kama mita 20 kutoka eneo la tukio nikatafuta usafiri wa piki piki nikaja kituoni hapa’.
Hizi ni picha za gari iliyosababisha ajali hiyo.2
1
Hizi ni picha za baadhi ya wanafunzi waliolazwa hospital ya mkoa wa Mtwara kufuatia ajali hiyo.
IMG-20140122-WA0007
IMG-20140122-WA0009
IMG-20140122-WA0004
IMG-20140122-WA0002
Hii ni taarifa ya Jeshi la polisi Mkoa wa Mtwara.
 press2
002

Story ikamilishe kwa kumsikiliza moja kati ya watoto waliokuwa kwenye ajali hiyo ambae amenusurika.

You Might Also Like

TPA watoa Elimu kuhusu huduma zao

Mkutano wa IAWP New Zealand wafungwa, CP Kaganda awakaribisha Wajumbe Tanzania

EWURA kutokomeza mafuta ya makopo vijijini

Mradi wa Umeme wa Upepo wa Zanzibar wapamba moto

Joe Biden atuma salamu za pole kwa Mfalme wa Morocco

Millard Ayo January 22, 2014
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Daraja la Dumila lasombwa na maji baadhi ya majengo ya Shule yafunikwa.
Next Article Jinsi wizara ya Fedha ilivyowapokea Mwigulu Nchemba na Malima leo January 22 2014.
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Watumishi watakiwa kujipanga kustaafu pindi wanapoajiriw.
Top Stories September 30, 2023
Anthony kurejea mazoezini baada ya sekeseke lililomkuta.
Top Stories September 30, 2023
TASAC kusisitiza matumizi sahihi ya vyombo vya majini.
Top Stories September 30, 2023
Maboresho ya bandari kusaidia ufanisi katika kazi.
Top Stories September 30, 2023

You Might also Like

Top Stories

Watumishi watakiwa kujipanga kustaafu pindi wanapoajiriw.

September 30, 2023
Top Stories

Anthony kurejea mazoezini baada ya sekeseke lililomkuta.

September 30, 2023
Top Stories

TASAC kusisitiza matumizi sahihi ya vyombo vya majini.

September 30, 2023
Top Stories

Askari polisi wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

September 29, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?