Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: TBS yatoa mafunzo ya sumukuvu kwa wadau wa mazao ya mahindi na karanga
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
March 26, 2023
Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”
March 26, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > TBS yatoa mafunzo ya sumukuvu kwa wadau wa mazao ya mahindi na karanga
Top Stories

TBS yatoa mafunzo ya sumukuvu kwa wadau wa mazao ya mahindi na karanga

November 24, 2021
Share
4 Min Read
SHARE

Serikali chini ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) imeanza rasmi kutoa mafunzo kupitia Mradi wa Kitaifa wa Kudhibiti Sumukuvu “Tanzania Initiative for Preventing Aflatoxin Contamination – TANIPAC” yanayotarajiwa kutolewa katika wilaya 18 zilizopo kwenye mikoa 10 nchini.

Mafunzo ya mradi huo yalizinduliwa rasmi Wilayani Kiteto mkoani Manyara na kuhudhuriwa na washiriki 120, ambapo mradi huo upo chini ya Wizara ya Kilimo na TBS imekabidhiwa jukumu la kutoa mafunzo hayo.

Akizungumzia na waandishi wa habari wilayani hapa kuhusu Wilaya na Mikoa itakayonufaika na mafunzo hayo Jabir Abdi wa TBS alitaja wilaya hizo kuwa ni za Kondoa, Chemba, Bahi, Kongwa, Babati, na Kiteto.

Wilaya zingine ni Namtumbo,Newala, Nanyumbu, Nzega, Urambo, Kibondo, Kasulu, Buchosa, Bukombe, Itilima, Kilosa na Gairo. Kuhusu mikoa zilizopo wilaya hizo, Abdi alisema ni Dodoma, Manyara, Ruvuma, Mtwara, Tabora, Kigoma, Mwanza, Geita, Simiyu na Morogoro.

Tafiti za awali za mradi huu zimebaini maeneo hayo tajwa kuwa kuna changamoto ya uwepo wa sumukuvu katika mnyororo wa thamani wa mazao ya mahindi na karanga na bidhaa zake.

Abdi aliwataja walengwa wa mafunzo hayo kuwa ni wafanyabiashara, wasafirishaji na wasindikaji wa mahindi na karanga pamoja na bidhaa zake.

Abdi alitaja faida za mafunzo kuwa yalenga kulinda afya za binadamu, kuwezesha biashara ya mazao ya mahindi na karanga, kulinda afya za mifugo na kuwezesha utoshelevu wa chakula salama.

Alitaja faida nyingine kuwa kuhimili ushindani katika masoko ya ndani, kikanda na nje ya nchi.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo jana Mkuu wa Wilaya ya Kiteto ndugu Mbaraka Alhaji Batenga, alipongeza uamuzi wa Serikali kuanzisha mafunzo hayo, kwa sababu chakula ni hitaji muhimu sana kwa binadamu na ustawi wa maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Hata hivyo, alisema usalama wa chakula unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na uchafuzi wa sumukuvu ambao husababisha madhara ya kiafya na hata kiuchumi.

Batenga, alisema sumukuvu huathiri zaidi mazao ya mahindi na karanga ambayo ni sehemu muhimu ya chakula cha Watanzania hapa nchini. “Kwa sababu hiyo sisi sote tunatakiwa kuzingatia mikakati ya kukabiliana na sumukuvu ili vyakula vyetu viendelee kuwa salama kwa muda wote,” Batenga.

Alifafanua kwamba anatambua nafasi ya wafanyabiashara, wasindikaji na wasafirishaji kwa ujumla wao na mchango wao walionao, hivyo serikaii imeandaa mafunzo hayo mahususi kwa ajili yao ili kuwajengea uwezo kwa ajili ya udhibiti sumukuvu.

Alisema umuhimu huu unasabishia suala la usalama wa chakula kupewa kipaumbele katika kulinda afya, jamii na uchumi wa nchi, kwa kuwa kigezo muhimu cha biashara kitaifa na kimataifa, kwani chakula kisicho salama husababisha madhara ya kiafya na vifo kwa walaji pamoja na athari za kiuchumi.

Alihimiza wadau hao kuzingatia mambo muhimu yanayoshauriwa na wataalam ili kudhibiti sumukuvu katika chakula, ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni bora za kilimo kama inavyoshauriwa na wataalam, kuvuna na kuondoa shambani mahindi na karanga mara baada ya kukomaa vizuri na kukaushia vizuri mazao yaliyovunwa kabla kuhifadhi.

Nyingine ni kuepuka kurundika mazao moja kwa moja kwenye sakafu, kuhakikisha wanahifadhi vizuri mazao na kwa lengo la kuepuka wadudu waharibifu, wanyama, joto kali na unyevunyevu.

You Might Also Like

Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM

Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’

Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake

Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza limefanya misa Takaridu ya Kumuombea Hayati JPM

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA November 24, 2021
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Rais Samia afunguka ‘Naitwa Bi Tozo, linanigusa ndani ya moyo’ (video+)
Next Article “Watakaopewa mimba ruksa kurudi shule” Ndalichako
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
Magazeti March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
Top Stories March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
Top Stories March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
Top Stories March 26, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM

March 26, 2023
Top Stories

Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’

March 26, 2023
Top Stories

Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”

March 26, 2023
Top Stories

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza limefanya misa Takaridu ya Kumuombea Hayati JPM

March 26, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?