Rais wa Ukraine anataka kukamilisha makubaliano ya mfumo wa uchimbaji wa madini ya Ukraine na kumuuliza mwenzake wa Marekani kama ana nia ya “kusitisha” msaada kwa Ukraine.
“Kuna tarehe ya kufanya kazi Ijumaa,” Bw. Zelensky ameeleza wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Kyiv.
“Swali langu (kwa Bw Trump) litakuwa la moja kwa moja: je, Marekani itasitisha msaada huo au la? Je, tunaweza kununua silaha, ikiwa hakutakuwa tena na msaada?”
Kwa upande wake Rais wa Marekani Donald Trump amesema anaridhia ziara inayoweza kufanywa na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy nchini humo.
Wanatarajiwa kusaini makubaliano yatakayoiruhusu Marekani kuchimba madini ya Ukraine.
Mazungumzo haya yanakuja baada ya utawala wa Trump kushangaza washirika wake wa Magharibi kwa kufanya mazungumzo ya kwanza ya ngazi ya juu na Moscow tangu Urusi ilipoivamia Ukraine zaidi ya miaka mitatu iliyopita.
Awali, Trump alionekana kumlaumu Zelensky kwa vita hivyo na kumkosoa kwa kushindwa kuanzisha mazungumzo ya amani mapema