Rais wa Marekani Donald Trump siku ya Jumanne alisema kuwa anapanga kurejesha kile alichokiita “shinikizo la juu”la sera dhidi ya Iran kwa madai kuwa inajaribu kutengeneza silaha za nyuklia na kudai kuwa anatumaini sera hiyo “italazimika kutumiwa.”
Trump alitoa maoni hayo alipokuwa akitia saini mkataba wa kurejesha sera kali ya vikwazo dhidi ya Iran, sawa na wakati wa muhula wake wa kwanza.
Mkataba huo unaagiza kila idara katika serikali ya Marekani kubuni vikwazo kwa Iran, hasa kuhusiana na shughuli za nyuklia, msaidizi wa White House alimwambia Trump katika hafla ya kutia saini.
Hii itampa Trump “zana zote zinazowezekana” kuzuia Iran kuwa “muigizaji mbaya,” msaidizi alisema.
Trump alionyesha masikitiko yake kwa hatua hizo kali, akisema: “Hii ni moja ambayo nimechanganyikiwa nayo. Kila mtu anataka niitie saini. Nitaifanya. Ni ngumu sana kwa Iran.”
“Natumai sitalazimika kuitumia sana,” alisema. “Sina furaha kufanya hivyo, lakini kwa kweli sina chaguo kubwa kwa sababu lazima tuwe na nguvu.”
“Tutaona kama tunaweza kupanga au la. Tutafanya makubaliano na Iran na kila mtu anaweza kuishi pamoja,” alisema.
Trump pia alitangaza kwamba ikiwa atauawa na Iran nchi hiyo “itaangamizwa.”