Chuo Kikuu cha Dar es Salaam- UDSM kinakualika katika maonesho ya wiki ya Utafiti na Ubunifu msimu wa 9 – 2024 yatakayofanyika 5 -7, June 2024 katika ukumbi wa Maktaba Mpya.
Akizungumza katika Ukaribisho huo, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo – Utafiti, Profesa Nelson Boniface amesema mwaka huu wamejipanga vyema hivyo washiriki wajitokeze kwa wingi.
Prof. Boniface amesema jumla ya Miradi 76 ilishinda katika maonesho ya awali, na katika Maonesho hayo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso.
Kauli mbiu; Kukuza utafiti na Ubunifu kupitia ubia baina ya chuo na taasisi mbali mbali.