Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: VANESSA BRYANT AMEKUBALI KULIPWA FIDIA YA $28.85MIL KUTOKANA NA KESI YA AJALI YA MUME WAKE.
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo May 30, 2023
May 30, 2023
Waziri Masauni asimama Bungeni Mei 29, 2023 ‘Watanzania 66 waukana Uraia’
May 29, 2023
Sentensi za Mkurugenzi wa Asas kwenye Mkutano Mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT)
May 29, 2023
Hospitali yachunguzwa kwa madai ya kuwaweka watoto wachanga kwenye maboksi
May 29, 2023
Marekani yabatilisha visa ya spika wa bunge la Uganda baada ya saini Mswada mkali wa ushoga kuwa sheria
May 29, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Entertainment > VANESSA BRYANT AMEKUBALI KULIPWA FIDIA YA $28.85MIL KUTOKANA NA KESI YA AJALI YA MUME WAKE.
Entertainment

VANESSA BRYANT AMEKUBALI KULIPWA FIDIA YA $28.85MIL KUTOKANA NA KESI YA AJALI YA MUME WAKE.

March 1, 2023
Share
3 Min Read
SHARE

Mke wa aliyekuwa nguli wa mpira wa kikapu Vanessa Bryant, amekubali kulipwa fidia ya $28,850,000 kutokana kesi ya madai aliyoifungulia Kaunti ya Los Angeles nchini Marekani, kutokana picha ambazo maafisa wa polisi wa Kanuti hiyo walizipiga na kuzisambaza baada ya ajali ya helikopta iliyomuua mume wake Kobe Bryant pamoja na binti yake Gianna mnamo Januari 2020, kulingana na mawakili wa kaunti. Mshtaki mwenza Chris Chester, ambaye mke wake na binti yake pia waliuawa kwenye ajali hiyo, wamekubali kulipwa $19,950,000.

Kutokana na taarifa iliyotolewa na wakili aliyesimamia kesi hiyo, alisema kuwa hii itakuwa kilele chenye mafanikio kwa Vanessa Bryant ambae alipigania haki ya mume wake, binti yake pamoja na wote waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo mbaya, huku walioshiriki kwenye vitendo hivyo visivyofaa wakiwajibishwa. Mawakili wa Kaunti ya LA walisema wanatumaini familia za Bryant na Chester zitaweza kupona kutokana na changamoto walizozipitia.

“Tunaamini kwamba suluhu iliyoidhinishwa na Bodi katika kesi ya Bryant ni ya haki na ya kuridhisha. Suluhu hio ya $28,850,000 linajumuisha uamuzi uliotolewa na mahakama ya shirikisho mnamo Agosti 2022 na kusuluhisha masuala yote ambayo bado hayajashughulikiwa yanayohusiana na madai ya kisheria yaliyosalia katika mahakama ya serikali, madai yoyote yaliyosalia kuhusiana na watoto wa Bryant na gharama nyinginezo, huku kila upande ukiwajibika kwa ada za mawakili wake,” Mira Hashmall, wakili mkuu wa kesi ya LA County katika kesi ya Bryant-Chester, alisema katika taarifa.

Kobe Bryant na binti yake Gianna, walikuwa wakielekea kwenye mechi ya mpira wa kikapu katika chuo chake cha michezo kiitwacho ‘Mamba Sports’ huko Thousand Oaks nchini Marekani pamoja na wengine waliokuwa wakisafiri nao mnamo Januari 26, 2020 wakati helikopta waliyokuwa wakisafiria ilipoanguka huko jijini Calabasas nchini Marekani. Watu wote tisa waliokuwa kwenye helicopter hiyo waliuawa.

Vanessa Bryant aliwasilisha kesi mahakamani miezi kadhaa baada ya ajali hiyo dhidi ya Kaunti ya Los Angeles, akidai kuwa maafisa wa Kaunti ya Los Angeles walichukua picha za mabaki ya binadamu waliopoteza maisha kwenye eneo la tukio kama “ukumbusho” na kuzisambaza huku akidai kuwa alipitia changamoto za kihisia na kuweweseka usiku na kuishtaki taasisi hiyo kwa uzembe na uvamizi wa haki za faragha. Mnamo Agosti 2022, mahakama ilimzawadia Vanessa Bryant dola milioni 16 kama fidia kutokana na kesi ya faragha dhidi ya Kaunti ya Los Angeles

You Might Also Like

Hospitali yachunguzwa kwa madai ya kuwaweka watoto wachanga kwenye maboksi

Marekani yabatilisha visa ya spika wa bunge la Uganda baada ya saini Mswada mkali wa ushoga kuwa sheria

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergey Lavrov azuru Kenya

July, 2022 hadi May, 2023 makosa makubwa ya jinai yameongezeka.

Cristiano Ronaldo kuondoka Al-Nassr adaiwa kuwasiliana na Real Madrid

TAGGED: TZA HABARI
Geena TZA March 1, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Good news kutoka kwenye maduka ya GSM, Punguzo la bidhaa kwa asilimia 30%, isikupite hii
Next Article Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa afunguka maeneo ya kijeshi yenye migogoro, aeleza sababu hii
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo May 30, 2023
Magazeti May 30, 2023
Waziri Masauni asimama Bungeni Mei 29, 2023 ‘Watanzania 66 waukana Uraia’
Top Stories May 29, 2023
Sentensi za Mkurugenzi wa Asas kwenye Mkutano Mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT)
Top Stories May 29, 2023
Hospitali yachunguzwa kwa madai ya kuwaweka watoto wachanga kwenye maboksi
Top Stories May 29, 2023

You Might also Like

Top Stories

Waziri Masauni asimama Bungeni Mei 29, 2023 ‘Watanzania 66 waukana Uraia’

May 29, 2023
Top Stories

Sentensi za Mkurugenzi wa Asas kwenye Mkutano Mkuu wa 37 wa Jumuiya ya Tawala za mitaa Tanzania (ALAT)

May 29, 2023

Marekani yabatilisha visa ya spika wa bunge la Uganda baada ya saini Mswada mkali wa ushoga kuwa sheria

May 29, 2023
Top Stories

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergey Lavrov azuru Kenya

May 29, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?