Heameda hospital imekuwa hospitali ya kwanza inayomilikiwa na Mtanzania mzalendo kufunga mitambo ya Cardiac Catheterisation (Cath Lab) ambayo inatoa huduma ya Matibabu ya moyo kwakutumia teknolojia ya kisasa
Mkurugenzi mkuu wa Heameda Hospital Dr. Kheri Mwandolela amesema kuwa mitambo hiyo inatumika kubaini na kutibu kuziba kwa mishipa ya damu, kutambua matundu kwenye moyo, kupima presha na magonjwa mengineyo yahusuyo Moyo.
Heameda inakuwa hospitali 5 nchini Tanzania kuwa na mashine yenye uwezo wa kutoa matibahu ya moyo pasipo mgonjwa kupasuliwa, ikiwa ni sehemu ya sekta binafsi kuunga mkono kwa vitendo jitihada za Mhe Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya Afya nchini.