Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Al-Nahla Group wawekeza dola milioni 120 kwa kampuni ya Smile Communications Tanzania
Share
Notification Show More
Latest News
Huyu ndie Kizz Daniel, Bilionea wa Buga, Mikasa ya Polisi mpaka kupelekwa Mahakamani
August 12, 2022
Basi la New Force latumbukia korongoni, Mmoja afariki, Polisi anena chanzo
August 12, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 12, 2022
August 12, 2022
PICHA: Matukio ya Mkutano Mkuu wa CAF uliyofanyika Tanzania
August 11, 2022
Ndugu abiria kulipwa Milioni 150, Wakili aibua mapya ‘Watu binafsi waliopost meme wajiandae’
August 11, 2022
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Al-Nahla Group wawekeza dola milioni 120 kwa kampuni ya Smile Communications Tanzania
Top Stories

Al-Nahla Group wawekeza dola milioni 120 kwa kampuni ya Smile Communications Tanzania

June 10, 2022
Share
4 Min Read
SHARE

Kampuni ya Smile Communications Tanzania inatarajia kupokea dola za kimarekani milioni 120 kutoka kampuni ya Al-Nahla Group ambayo kwa sasa inamiliki asilimia 100 ya kampuni hiyo kupitia miongoni mwa kampuni zake iitwayo 966 Co. S.a.r.l ambapo hii ni baada ya uongozi wa kampuni za Al-Nahla Group na kampuni ya Smile Telecom Holding ambayo inafanya kazi kwenye nchi zikiwemo Tanzania, Nigeria, Uganda na DR Congo kukubaliana kujiimarisha kwa lengo ka kuongeza utoaji huduma nchini Tanzania.

“Uwekezaji huu kwetu ni jambo la furaha na matumaini yetu ni kwamba uwekezaji huu utakuwa chachu ya utoaji huduma zetu kwenye soko la mawasiliano na unaendana na dira na mkakati wetu. Uwekezaji wetu utachangia upatikanaji wa huduma za mawasiliano endelevu yaani 4G LTE kwa watu wote wanaoishi nchini Tanzania na utaleta manufaa makubwa ya kijamii kwa watumiaji” alisema Bw Ahmad Farroukh, Mkurugenzi Mtendaji wa Smile Group na Mwenyekiti wa bodi ya Tanzania.


Aliongeza kuwa “Uwekezaji huu utatengeneza fursa nyingi zaidi kwa Watanzania katika nyanja ya ushirikishwaji wa kidijitali huku akisisitiza kuwa kampuni ya Smile Communications imekuwa ikipanua shughuli zake, na kwa sasa huduma zake zinapatikana maeneo mengi nchini katika kipindi cha miaka miwili iliyopita huku nakuongeza kuwa idadi ya wateja wake imekuwa pia na kusistitza kuwa baada ya kukamilisha mpango wa kimkakati wa kujiimarisha ambao ulitangazwa mnano febuari 2022, kampuni yake imeendelea kutoa huduma kama kawaida na kusema ufadhili mpya itasaidia kamuni ya Smile Telecoms Group kujiimarisha zaidi, kuongeza wigo na kutimiza malengo yake ya kibiashara.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Smile Communications nchini Tanzania Zuweina Farah, kampuni itatoa kipaumbele kuwezesha upatikanaji wa huduma zenye kasi zaidi na za kimataifa za mtandao na sauti “Tumewekeza katika uundaji upya na upanuzi wa mtandao wetu ili kuwapa wateja wetu huduma zilizoboreshwa za mtandao na kasi zaidi. Ukuaji wa wateja wa Smile katika kipindi cha miaka miwili iliyopita umekuwa mzuri sana, na tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora na za uhakika kwa wateja wetu” alisema Bi. Zuweina Farah.


Aliongeza kuwa kampuni yake inatarajia kupanua huduma zake nchi nzima huku akitoa shukrani kwa Serikali ya Tanzania, hususan Wizara ya TEHAMA, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kwa kazi nzuri waliyoifanya na kuendelea kuungwa mkono juhudi za kampuni yake.

“Tumejizatiti kuendelea kutoa huduma bora za mawasiliano nchini Tanzania. Wateja wetu waendelea kutunga mkono na wategemee mengi mazuri kutoka kwetu,” alisema Farah.

Kampuni ya Al Nahla Group lilianzishwa na marehemu H.E. Hassan Abbas Sharbatly, ambaye hapo awali alianzisha Benki ya Riyad. Leo kampuni hiyo inamiliki hisa asilimia 9 ya Benki ya Riyad, iliyoorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Saudi.

Kampuni hiyo ya kifamilia inaangazia sekta za magari, mali isiyohamishika, biashara, biashara za baharini, nishati mbadala, mawasiliano ya simu na uwekezaji. Uwekezaji wake unalenga Falme za Kiarabu (Saudi Arabia), Ghuba, Misri na sekta chache za viwanda barani Afrika, pamoja na Smile Telecom Holding Group ikiwa ni mmoja wao.

You Might Also Like

Basi la New Force latumbukia korongoni, Mmoja afariki, Polisi anena chanzo

Ndugu abiria kulipwa Milioni 150, Wakili aibua mapya ‘Watu binafsi waliopost meme wajiandae’

Ajali Mbaya!! Watu sita wafariki, Polisi wafunguka, chanzo ‘Dereva alikuwa Mwendokasi, lilipinduka’

Hafla ya makabidhiano ya data za utafutaji wa Mafuta na Gesi asilia kwa vitalu Zanzibar

Ukumbini: Bwana Harusi aonesha video ya mkewe akiwa faragha na shemeji yake chumbani

TAGGED: TZA HABARI
Millard Ayo June 10, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Wafanyabiashara Mwanza wakutanishwa na Akiba Commercial Bank
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 11, 2022
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Huyu ndie Kizz Daniel, Bilionea wa Buga, Mikasa ya Polisi mpaka kupelekwa Mahakamani
Entertainment August 12, 2022
Basi la New Force latumbukia korongoni, Mmoja afariki, Polisi anena chanzo
Top Stories August 12, 2022
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 12, 2022
Magazeti August 12, 2022
PICHA: Matukio ya Mkutano Mkuu wa CAF uliyofanyika Tanzania
Sports August 11, 2022

You Might also Like

Sports

Kauli ya Simba SC baada ya Tundaman kuingia na Jeneza ‘Simba day’ uwanja wa Mkapa

August 10, 2022
Sports

Picha 19: Uzinduzi wa Jezi mpya za Simba SC, Mashabiki wafurika Dukani DSM

August 7, 2022
Sports

Simba wafunga usajili kwa kishindo, washusha mshambuliaji kutoka Ulaya

August 7, 2022
Sports

Manara amuingiza Hersi kwenye 18 za TFF

August 7, 2022
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?