Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Wafanyabiashara waahidi kusajili majengo ya chakula na vipodozi
Share
Notification Show More
Latest News
Mwili waopolewa mto Msimbazi DSM, Jeshi la Zimamoto (VideO+)
March 22, 2023
Rais Samia atoa Bilioni 196.6 Mlele Kwa miaka miwili
March 22, 2023
Video: Rais Samia amuibua Ally Hapi, Afunguka haya
March 22, 2023
Mfungo wa Ramadhan Kaya 1000 zapatiwa vyakula “Tunarudisha kwa Jamii”
March 22, 2023
Jamaa aangusha gari Mtaroni, Dereva haonekani, mashuhuda wasimulia, ‘Alikuwa anaongea na simu’
March 22, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Wafanyabiashara waahidi kusajili majengo ya chakula na vipodozi
Top Stories

Wafanyabiashara waahidi kusajili majengo ya chakula na vipodozi

September 7, 2021
Share
4 Min Read
SHARE

Wafanyabiashara na wajasiriamali mkoani Lindi wamepata mwamko wa kuthibitisha ubora wa bidhaa zao pamoja na kusajili majengo ya chakula na vipodozi kupitia elimu ambayo imetolewa na maofisa wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuanzia Agosti 31 hadi Septemba 6, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Lindi kuhusiana na majumuisha ya kazi ambayo maofisa wa shirika hilo wamefanya katika wilaya tatu za mkoa huo, Afisa Usalama wa Chakula wa TBS, Barnabas Jacob, alisema wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa sababu wamefikia walengwa wengi.

“Tumeweza kufikia welengwa wengi tuliokuwa tukiwatarajia katika Wilaya za Liwale, Nachingwea na Lindi na wameahidi kujitokeza kuthibitisha ubora wa bidhaa zao pamoja na kusajili majengo ya chakula na vipodozi ili waweze kuendesha shughuli zao kwa mujibu wa sheria,”  Jacob.

Jacob alisema katika Wilaya hizo wamefanya ukaguzi kwenye maduka ya vyakula na vipodozi, kutembelea wajasiriamali wadogo wanaofanya uzalishaji wa bidhaa ili kuwahamasisha kupata alama ya ubora.

Alisema katika Wilaya ya Lindi wajasiriamali 18 wameahidi kuanza mchakato wa kuthibitisha ubora zao.

Alisema wilayani Lindi wametoa elimu kwa umma kwa watumishi la Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kuhusu madhara ya matumizi ya bidhaa hafifu, hususani vipodozi ambavyo vimekatazwa kutumika nchini kutokana na kuwa na viambata sumu vyenye madhara kwa afya za watumiaji

Kwa upande wa Wilaya ya Nachingwea watumishi waliopatiwa elimu hiyo ni wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), TRA, Benki ya Biashara Tanzania (TCB), TTCL na wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Jacob alifafanua kwamba elimu hiyo itawawezesha watumishi hao kuwa mabalozi wazuri ndani ya jamii na familia zao kwa ujumla.

Alisema elimu hii imelenga taasisi za umma ikiwa ni mwendelezo wa shirika kutoa elimu kwa umma kuhusiana na madhara ya vipodozi na vyakula vilivyopigwa marufuku,” alisema Jacob na kuongeza;

“Watumishi katika taasisi ambazo tumetoa elimu wamepata mwamko mkubwa na wametuahidi kuwa mabalozi kwa watu wengine ikiwemo familia na jumuiya zinazowazunguka kuhusiana na madhara ya vipodozi hivyo,” Jacob.

Kama ilivyo kuwa kwa Wilaya ya Lindi, Jacob alisema na Nachingwea walitembelea viwanda ambavyo vimethibitishwa na TBS ili kuangalia kama vinaendelea kuzalisha bidhaa kwa mujibu wa viwango walivyopewa.

“Kimsingi tumetoa elimu ya kutosha kwa wazalishaji wa bidhaa ili waweze kufanya usajili wa majengo yao ya bidhaa za vyakula na vipodozi na kuhamasisha wajasiriamali ili waje kupata alama ya ubora kwa kupitia SIDO,” Jacob.

Kwa upande wa Liwale, Jacob alisema mbali na kutoa elimu kwa wajasiriamali na wafanyabiashara, walifanya ukaguzi wa awali kwa wenye viwanda ambavyo wazalishaji wake wanataka kupata alama ya ubora.

Alitaja miongoni mwa viwanda ambavyo maofisa hao wa TBS wamefanya ukaguzi na kuhamasisha kujitokeza kupata alama ya ubora kuwa ni pamoja na vile vinavyokamua mafuta ya alizeti, viwanda vya kubangua korosho, kwenye mashine za kusaga unga pamoja na kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za mikate.

“Wote hao tumewafikia na kuwahamasisha kuja kupata alama ya ubora TBS” alisema Jacob.

Aidha, alitaja kazi nyingine ambayo wameifanya wilayani humo kuwa ni pamoja na kukagua na kusajili maduka ya vipodozi na chakula ili kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa kukidhi matakwa ya sheria za nchi na kulinda afya za walaji.

You Might Also Like

Mwili waopolewa mto Msimbazi DSM, Jeshi la Zimamoto (VideO+)

Rais Samia atoa Bilioni 196.6 Mlele Kwa miaka miwili

Video: Rais Samia amuibua Ally Hapi, Afunguka haya

Mfungo wa Ramadhan Kaya 1000 zapatiwa vyakula “Tunarudisha kwa Jamii”

Jamaa aangusha gari Mtaroni, Dereva haonekani, mashuhuda wasimulia, ‘Alikuwa anaongea na simu’

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA September 7, 2021
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Marioo katuletea wimbo mpya “Beer tamu” unaweza ukausikiliza hapa
Next Article Tazama Petro wa CCM alivyowaacha hoi ukumbini, Rais Samia ahudhuria ibada ya ndoa yake (video+)
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Mwili waopolewa mto Msimbazi DSM, Jeshi la Zimamoto (VideO+)
Top Stories March 22, 2023
Rais Samia atoa Bilioni 196.6 Mlele Kwa miaka miwili
Top Stories March 22, 2023
Video: Rais Samia amuibua Ally Hapi, Afunguka haya
Top Stories March 22, 2023
Mfungo wa Ramadhan Kaya 1000 zapatiwa vyakula “Tunarudisha kwa Jamii”
Top Stories March 22, 2023

You Might also Like

Top Stories

Mwili waopolewa mto Msimbazi DSM, Jeshi la Zimamoto (VideO+)

March 22, 2023
Top Stories

Rais Samia atoa Bilioni 196.6 Mlele Kwa miaka miwili

March 22, 2023
Top Stories

Video: Rais Samia amuibua Ally Hapi, Afunguka haya

March 22, 2023
Top Stories

Jamaa aangusha gari Mtaroni, Dereva haonekani, mashuhuda wasimulia, ‘Alikuwa anaongea na simu’

March 22, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?