Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Wanafunzi Sekondari 7,457, Msingi 1,554 wapata ujauzito
Share
Notification Show More
Latest News
MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
March 24, 2023
Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’
March 24, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > Wanafunzi Sekondari 7,457, Msingi 1,554 wapata ujauzito
Top Stories

Wanafunzi Sekondari 7,457, Msingi 1,554 wapata ujauzito

February 1, 2023
Share
2 Min Read
SHARE

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imelieleza Bunge kuwa katika kipindi cha mwaka 2021 na 2022 wanafunzi 1,554 wa shule za msingi na 7,457 wa sekondari walipata ujauzito.

Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson alisema takwimu hizo ni kubwa. Akaitaka hiyo wizara kuandaa takwimu kuhusu idadi ya wanaume walioshitakiwa na kupatikana na hatia ya kuwapa ujauzito wanafunzi.

Dk Tulia alisema takwimu kuhusu wanaume wenye hatia ni muhimu ili kuona kama sheria ya kuwalinda watoto dhidi ya vitendo viovu inafanya kazi.

Awali wakati akijibu swali la wali la Mbunge wa Viti  Maalumu, Hawa Chakoma (CCM), Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Omari Kipanga alisema bungeni Dodoma kuwa, wanafunzi 1,692 wa shule za sekondari wamerejeshwa shuleni baada ya kukatiza masomo kwa sababu ya ujauzito. Mbunge huyo aliuliza ni wanafunzi wangapi waliokuwa wajawa zito na wangapi wamerejeshwa shuleni baada ya agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuwataka wanafunzi wote waliopata ujauzito wakiwa shuleni warejeshwe.

Kipanga alisema idadi hiyo ni waliorudi shuleni hadi kufikia Januari mwaka huu na akasema wanaendelea kukusanya takwimu za shule za msingi.

Alisema ili kumaliza tatizo hilo serikali imeweka mikakati minne ukiwemo wa Rais Samia kuridhia kujengwa shule 26 za sekondari za wasichana moja kila mkoa.

Kipanga alisema pia mkakati wa serikali ni kuhakikisha kwamba ujenzi wa hosteli unaendelea kwenye maeneo yenye umuhimu wa kuwa na mabweni.

Aliwaeleza wabunge kuwa mkakati mwingine wa serikali ni kuanzisha vitengo vya elimu ya unasihi na ushauri katika shule mbalimbali ili kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji havijitokezi. Pia mkakati mwingine ni kuchukua hatua kwa wale wote wanaohusika katika vitendo vya kunyanyasa wanafunzi ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

Kuhusu kutunga sheria, Kipanga alisema, ni kweli kuna waraka namba 2 wa 2021 wa urejeshaji wanafunzi na ni mwaka mmoja tangu umetoka hivyo wanaendelea kufanya tathmini ya utekelezaji wake na changamoto na mafanikio yaliyopo.

You Might Also Like

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

TAGGED: TZA HABARI
Pascal Mwakyoma TZA February 1, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Dizeli, mafuta ya taa yashuka bei
Next Article ‘Ondoeni dhana ya rushwa Mahakamani’
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.
Top Stories March 24, 2023
China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.
Top Stories March 24, 2023
20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.
Top Stories March 24, 2023
INDIA: Sheria mpya, kutobadili imani ya kidini yazua gumzo.
Top Stories March 24, 2023

You Might also Like

Top Stories

MAREKANI:Makamu wa rais Kamala Harris kukutana na viongozi wa Ghana, Tanzania na Zambia.

March 24, 2023
Top Stories

China yapinga uuzwaji wa sehemu ya programu yake “TikTok” kwa kulazimishwa na kutishiwa kufungiwa.

March 24, 2023
Top Stories

20 wafariki kutokana na virusi vya Marburg nchini E.Guinea.

March 24, 2023
Top Stories

Ndoa za jinsia moja zamuibua Makamu wa Rais, atoa tamko ‘hata wanyama hawafanyi’

March 24, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?