Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Watu wenye ulemavu wapongeza jitihada za serikali
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
March 26, 2023
Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”
March 26, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Mix > Watu wenye ulemavu wapongeza jitihada za serikali
Mix

Watu wenye ulemavu wapongeza jitihada za serikali

September 7, 2022
Share
3 Min Read
SHARE

Watu wenye ulemavu wameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza kasi ya kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Pongezi hizo zilitolewa jijini Dodoma, mbele ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu Pro. Jamal Katundu wakati akipokea vifaa vya watu wenye ulemavu kutoka Taasisi ya ASA Microfinance.

Amesema vifaa vilivyopokelewa ni viti mwendo pisi 35, mafuta maalumu kwa ajili ya watu wenye ualbino 35 na fimbo maalumu kwa watu wenye matatizo ya kuona 35.

“ASA mmekuwa mkitoa misaada mbalimbali kwa ajili ya watu wenyeulemavu na tumekuwa tukitumia nafasi hii kuwaomba wadau wengine kuiga mfano wenu pia mmeendelea kushirikiana na serikali kutoa huduma kwa watu wenye mahitaji maalumu si jambo dogo kwa leo tutapokea viti mwendo pisi 35 mafuta kwa ajili ya watu wenye ualubino 35 na fimbo maalumu 35,”alisema

Profesa Katundu alisema serikali inaendelea kuhamasisha taasisi nyingine kuiga mfano katika kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu ili kuimarisha maendeleo yao, ustawi na taifa kwa ujumla.

Kwa Upande wake Mwanasheria wa Taasisi ya ASA microfinance Zephania Paul alisema vifaa vilivyotolewa na asasi hiyo vinathamani ya Tsh. Milioni 13.5 huku akisisitiza kuwa lengo ni kuona umuhimu wa kuishi na watu wenye mahitaji maalumu kwa kichache kinachopatikana.

“Taasisi yetu ya ASA imekuwa ikifanya hivy mara kwa mara kwa lengo la kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuhakikisha anawaboreshea maisha Watu wenye Ulemavu nchini,”alisema

Akizungumza awali, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye ulemavu Mkoa wa Dodoma, Omary Lubuva amempongeza Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan kwa hatua mbalimbali anazochukua katika kutatua changamoto zao na kuhakikisha wanashirikishwa katika shughuli mbalimbali za kukuza uchumi.

Ameongeza kuwa msaada huo waliopata ni muhimu kwani utawawezesha watu wenye ulemavu kujimudu na kushiriki kwenye shughuli mbalimbali.

“Sisi Watu wenye Ulemavu tunatambua na kuthamini jitihada na juhudu zinazofanywa na serikali yetu inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia katika kutatua changamoto zetu, tunaomba taasisi na asasi nyingine waweze kuona haya ambayo yanafanywa na baadhi ya wenzao ili na wao waone wanawezaje kushiriki katika kusaidia kuboresha masha yetu,” alisema

Naye, Bi. Sophia Mhando (mwenye ulemavu wa Miguu) amesema hajawahi kufikiri kuwa ipo siku atapata kiti mwendo kwa kuwa amekuwa akihangaika kutembea na kuomba omba hivyo kupata kiti mwendo hicho kitamwezesha kujishughulisha na shughuli za ujasiriamali.

You Might Also Like

USAID Breakthrough ACTION Launches SPARK Program

Wataalam wa maji watoa wito wa kukabiliana na uhaba wa maji

Kamati ya Bunge ya Miundombinu imeridhishwa na ujenzi wa BRT

Waziri Mkuu awataka vijana na Wanawake kuchangamkia program ya IMBEJU

AudioMPYA: Joshua Ngelendo anakualika kusikiliza “Jemedari”

TAGGED: habaridaily
Rama Mwelondo TZA September 7, 2022
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Mchungaji aliyefariki dunia agosti 2021 bado hajafufuka, mpaka sasa yupo ndani chumba cha kuhifadhia maiti
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo September 7, 2022
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 27, 2023
Magazeti March 27, 2023
Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM
Top Stories March 26, 2023
Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’
Top Stories March 26, 2023
Picha: Mfugaji akamilisha Mjengo wake, aishukuru Kampuni ya Asas kwa kufanikisha ndoto zake
Top Stories March 26, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Kutoka kwenye Usiku wa Malkia wa nguvu Mlimani City Hall DSM

March 26, 2023
Top Stories

Hhayuma afunguka uwepo wa Baraza la ardhi Hanang, ‘Nilitaka kushika Shilingi ya Waziri Bungeni’

March 26, 2023
Top Stories

Waziri Jafo acharuka, atoa maagizo Mbweni “Wachimba Mchanga, kamata gari, hatua zichukuliwe”

March 26, 2023
Top Stories

Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza limefanya misa Takaridu ya Kumuombea Hayati JPM

March 26, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?