Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: WAZIRI MCHENGERWA AZINDUA MAGARI 22 YA DORIA TAWA, AHIMIZA KUCHAPA KAZI.
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 3, 2023
June 3, 2023
Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’
June 2, 2023
Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi
June 2, 2023
Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.
June 2, 2023
Nyota wa zamani wa Manchester United Lingard kuondoka Nottingham Forest
June 2, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Top Stories > WAZIRI MCHENGERWA AZINDUA MAGARI 22 YA DORIA TAWA, AHIMIZA KUCHAPA KAZI.
Top Stories

WAZIRI MCHENGERWA AZINDUA MAGARI 22 YA DORIA TAWA, AHIMIZA KUCHAPA KAZI.

February 17, 2023
Share
2 Min Read
SHARE

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa (Mb) leo Februari 16, 2023 amezindua magari 22 ya TAWA yatakayotumika Kwa ajili ya shughuli za doria na kudhibiti Wanyamapori Wakali na Waharibifu.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa magari hayo iliyofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya TAWA Mkoani Morogoro Mhe. Mchengerwa ameushukuru uongozi wa TAWA Kwa kutenga fedha ambazo zimewezesha kununua magari hayo ambayo yatatumika katika shughuli za doria, kudhibiti ujangili na Wanyamapori Wakali na Waharibifu.

Waziri Mchengerwa amesema mbali na shughuli za kudhibiti ujangili, magari hayo yatumike pia katika kujenga mahusiano mazuri na Wananchi wanaozunguka maeneo ya hifadhi.

Mhe. Mchengerwa ameagiza watumishi wa Wizara yake kujipanga katika kuhifadhi rasilimali za Nchi hii, kuongeza Kasi ya kutangaza Vivutio vya Utalii vilivyopo Nchini na kufanya kazi Kwa bidii.

“…Tujipange kwenda kuhifadhi sana, tuhifadhi kwelikweli, zile changamoto tunazoweza kuzitatua ni Lazima tuzitatue” amesema

“Nitataka Kila mmoja wetu akafanye kazi kwenye eneo lake, na afanye kazi kwelikweli, kama utatakiwa kuwepo kwenye eneo lako Saa sita mchana uwepo kwenye eneo lako” amesisitiza Waziri Mchengerwa.

Ameongeza kusema pamoja na kazi nzuri za kuhifadhi zinazofanywa na TAWA na Taasisi zingine za Uhifadhi bado asilimia 21 ya pato la Taifa linalochangiwa na Wizara ya Maliasili ni dogo kulinganishwa na wingi wa rasilimali zilizopo katika Taifa hili, hivyo amehimiza kuongeza kasi ya kutangaza vivutio vya Utalii Ili kuongeza pato la Taifa.

Hii ni ziara ya kwanza ya Mhe. Waziri Mchengerwa tangu kuteuliwa kwake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii ambapo aliongoza na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Hassan Abbas Said ambaye nae aliteuliwa hivi Karibuni.

Wengine waliongozana na Waziri Mchengerwa ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb), Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Juma Mkomi,
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bi Prisca Lwangili na Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori , Dkt. Maurus Msuha.

You Might Also Like

Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’

Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi

Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.

Serikali ya Congo na mahakama ya ICC zakubaliana kuimarisha ushirikiano

Amnesty yaonya Iran dhidi ya Kunyonga kwa Kesi zinazohusiana na madawa ya kulevya

Millard Ayo February 17, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Habari kubwa Magazetini Kenya leo February 17, 2023
Next Article RC Tanga awataka Viongozi wa Mkoa kuongeza Ufaulu Mashuleni
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 3, 2023
Magazeti June 3, 2023
Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’
Top Stories June 2, 2023
Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi
Top Stories June 2, 2023
Mlipuko wa ugonjwa wa Marburg umekwisha rasmi Tanzania.
Top Stories June 2, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: DC Halima Bulembo aungana na wakuu wa Idara, ‘Kutekeleza wajibu wao katika Utumishi’

June 2, 2023
Top Stories

Upinzani unashinikiza mageuzi mapya ya uchaguzi

June 2, 2023
Sports

Nyota wa zamani wa Manchester United Lingard kuondoka Nottingham Forest

June 2, 2023
Top Stories

Serikali ya Congo na mahakama ya ICC zakubaliana kuimarisha ushirikiano

June 2, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?