Millard AyoMillard Ayo
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
  • Contact
Search
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Reading: Waziri Mkuu awataka vijana na Wanawake kuchangamkia program ya IMBEJU
Share
Notification Show More
Latest News
Habari kubwa Magazetini Kenya leo June 4, 2023
June 4, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 4, 2023
June 4, 2023
Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia
June 3, 2023
Mapokezi ya ndege ya kwanza ya mizigo aina ya Boeing 767 -300F
June 3, 2023
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuapishwa kuliongoza taifa hilo
June 3, 2023
Aa
Millard AyoMillard Ayo
Aa
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Search
  • Top Stories
  • Entertainment
  • Sports
  • Magazeti
Follow US
  • Contact
  • Blog
  • Complaint
  • Advertise
© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.
Millard Ayo > Blog > Mix > Waziri Mkuu awataka vijana na Wanawake kuchangamkia program ya IMBEJU
Mix

Waziri Mkuu awataka vijana na Wanawake kuchangamkia program ya IMBEJU

March 11, 2023
Share
2 Min Read
SHARE
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo ametoa rai kwa vijana na wanawake kote nchini kuchangamkia programu ya uwezeshaji kiuchumi iliyozinduliwa na Benki ya CRDB kwa kushirikiana na Tume ya TEHAMA (ICTC), na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kuboresha bunifu zao za kibiashara.
Waziri Mkuu ametoa rai hiyo wakati wa Semina ya Uwekezaji na Fedha ya Benki ya CRDB maarufu kama “CRDB Bank Uwekezaji Day” iliyoenda sambamba na uzinduzi wa taasisi ya hisani ya CRDB Bank Foundation, pamoja na programu hiyo ya iMBEJU ambayo inalenga kutoa mafunzo, ushauri, na mitaji wezeshi kwa vijana na wanawake.
Waziri Mkuu amesema programu hiyo imekuja kutoa suluhisho kamili kwa biashara changa za vijana na wanawake nchini kwa kuzijengea uwezo wa kujiendesha hususani kupitia mafunzo ya kimkakati ambayo yamepangwa kutolewa kwa kushirikiana na ICTC, COSTECH, pamoja na wadau wengine katika programu za uwezeshaji wanawake kupitia vikundi.
“Ukweli ni kuwa tatizo la kushindwa kuendelea kwa biashara changa si kukosekana kwa mitaji. Mitaji ipo na taasisi zetu za fedha zipo tayari kufadhili, lakini hatari ya uchechefu ni kubwa kwani biashara changa nyingi zimekuwa zikishindwa kujisimamia. Niwashukuru Benki ya CRDB kwa kuliona hili na kuambatanisha programu ya iMBEJU na ushauri na mafunzo,” alisema.
Waziri Mkuu aliwataka vijana na wanawake kutumia vizuri mitaji watakayopewa kwa kuwekeza katika maeneo waliyoyaainisha kupitia mipango yao ya biashara, huku akiwasisitiza kuwa waaminifu. Alizitaka pia taasisi za Serikali kutoa fursa kwa vijana waliokuja na bunifu zinazoweza kutatua changamoto za jamii, akitolea mfano wa vijana waliobuni mfumo wa kuongoza magari barabarani kupewa fursa na Wizara ya Ujenzi.
Waziri Mkuu aliipongeza Benki ya CRDB kwa kuja na programu hiyo, na kusema inaendana na dira ya serikali ya kuchochea ubunifu kwa vijana na wanawake ili kutengeneza ajira, na kuchochea maendeleo nchini. Waziri Mkuu aliwahakikishia vijana kuwa Serikali ipo pamoja nao katika kufanikisha bunifu zao zinakuwa na tija kwao na kwa jamii kwa ujumla.

You Might Also Like

Hifadhi ya Mpanga Kipengere kusherehekea siku ya Maanguko ya Maji Duniani

Wabunge wafurahishwa na utekelezwaji wa mradi wa bomba la mafuta ghafi EACOP

Profesa Mkenda kufungua maonesho ya Nane ya Tafiti na Ubunifu UDSM

Miaka 5 ya ITM, Serikali imeahidi kuadhimisha sekta ya rasilimali watu

Yanga, UNICEF na Serikali zaungana kutoa elimu Ugonjwa wa Kipindupindu

TAGGED: habaridaily
Rama Mwelondo TZA March 11, 2023
Share this Article
Facebook TwitterEmail Print
Share
Previous Article Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson aongoza kikao cha Kundi la SADC
Next Article Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo March 11, 2023
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

You must be logged in to post a comment.

- Advertisement -

Latest News

Habari kubwa Magazetini Kenya leo June 4, 2023
Magazeti June 4, 2023
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo June 4, 2023
Magazeti June 4, 2023
Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia
Top Stories June 3, 2023
Mapokezi ya ndege ya kwanza ya mizigo aina ya Boeing 767 -300F
Top Stories June 3, 2023

You Might also Like

Top Stories

Picha: Kutoka Airport DSM, Ndege ya kwanza ya mizigo ‘Boeing 767-300F ilivyotua, Rais ashuhudia

June 3, 2023
Top Stories

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatarajiwa kuapishwa kuliongoza taifa hilo

June 3, 2023
Top Stories

Watu 288 sasa wamethibitishwa kufarikiwengine 900 kujeruhiwa katika ajali ya treni India

June 3, 2023
Top Stories

Ukraine iko tayari kuzindua mashambulizi-Volodymyr Zelensky

June 3, 2023
Show More
//

To be recognized as Africa’s leading and most trusted online media network providing quality content across all our media platforms by 2025

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

Millard AyoMillard Ayo
Follow US

© 2022 MILLARD AYO. Designed by F&A. All Rights Reserved.

Removed from reading list

Undo

Lost your password?