Shirika la Bima Zanzibar (ZIC), limeibuka mshindi katika kipengele cha shirika la bima la kuaminika zaidi (Most Reliable Insurance Corporation) katika tuzo zinazotolewa kila mwaka na Jarida la Global Brands la Uingereza.
Katika orodha iliyotolewa leo ya washindi mbalimbali wa tuzo hizo, chapa ya ZIC imeonekana kuwa iliyoaminika zaidi kwa mwaka 2023 upande wa sekta ya bima.
Wakati ZIC ikiibuka mshindi katika kipengele hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Arafat Haji ameibuka mshindi wa tuzo ya Mtendaji Bora wa Sekta ya Bima kwa mwaka 2023 ya jarida hilo.
Akizungumzia ushindi wake a ZIC katika tuzo hizo, Arafat meema kuwa umetokana na juhudi za pamoja za kuhakikisha shirika hilo linapiga hatua.
“Nimefurahia kupigiwa kura kuwa Mkurugenzi Mtendaji Bora wa Mwaka wa Shirika la Bima na ZIC kama Kampuni ya Bima inayotegemewa zaidi Tanzania katika tuzo zinazotolewa na Global Brands
Magazine.
“Haya ni matokeo ya Uchapakazi na kujitolea kwa timu nzima ya ZIC na Bodi yetu,” amesema Arafat.
Global Brands ni jarida ambalo limekuwa likijihusisha na utoaji habari na tuzo mbalimbali zinazohusu chapa za sekta tofauti duniani.