Ni video ya Mfalme wa Taarab Mzee Yusufu ya wimbo wa mpenzi Chokolate, video imegharimu jumla ya shilingi milioni nane za kibongo.

Helkopta ilipaa mara mbili hewani kwa muda kama wa dakika tatu na kutua pale Sea Cliff Dar es salaam

.

.

.

.

.

.

.

.

Millard Ayo na Mzee Yusuf, Interview Exclusive itasikika kwenye AMPLIFAYA Jumatatu.

.

TAARIFA MPYA ZA MWIGIZAJI SAJUKI KUTOKA INDIA.

Posted: 19th May 2012 by MillardAyo in News

Wastara.

Mke wa Sajuki (Wastara) ambae yuko India kwa sasa akiwa anamuuguza mumewe (Sajuki) amezungumza kwa mara ya kwanza na millardayo.com kuhusu hali ya sasa ya Sajuki.

Amesema “kwa kweli hali imebadilika na ninategemea kuona hali nzuri zaidi leo ni siku ya tano toka tumekuja huku India, Sajuki amebadilika sana kwa sababu siku tulipoondoka Tanzania hali yake ilikua mbaya hata rangi alibadilika lakini kwa sasa amerudi kwenye hali ya kawaida”

Kwenye sentensi nyingine, Wastara amesema Sajuki alikua hawezi hata kuongea ukamuelewa, sasa hivi anaongea hata kwa mda wa saa moja kitu ambacho alikua hawezi kabisa na sasa hivi ameweza kukaa kabisa”

Sajuki alipokua akisafirishwa kwenda India.

Wastara amesema “changamoto tuliyonayo ni kwamba tunahudumiwa na watu mbalimbali ukiachana na dokta, hawajui kingereza sasa unaweza kukuta unahitaji kitu lakini hamuelewani, kitu kingine ni swala la chakula, chakula ni kipya kwetu wote wawili huku ni Asia wana vyakula vyao”

Kuhusu Ugonjwa wa Sajuki, Wastara amesema walivyoondoka Tanzania walijua wanakwenda India na Sajuki atatibiwa ugonjwa unaomsumbua moja kwa moja lakini kabla ya kufanyiwa chochote ikagundulika kwamba alikua na tatizo la pumzi hivyo haikuwezekana kutibiwa ugonjwa wake kwa sababu inatakiwa kabla ya kufanyiwa opareshen anatakiwa kuwa kwenye hali ya kawaida, kwa hiyo ametibiwa kwanza tatizo la pumzi ili aweze kuhema vizuri ndio aanze kutibiwa ugonjwa wake”

Kwa kumalizia Wastara amesema “mimi pia nilipofika tu India nilikua mdhaifu, nilipoteza Network zote ikabidi nilazwe kwa sababu nilikua hoi, hapa yenyewe nimelazwa lakini naendelea vizuri”

.

.

.

.

.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 19

Posted: 19th May 2012 by MillardAyo in News

Hii ndio nyumba anayomiliki baba yake Kanumba huko Ngokolo Shinyanga, sehemu ya nyumba amepangishia watu wengine

Mimi nikifanya mahojiano na baba Kanumba ambae nilimfungia safari mpaka Shinyanga.

.

Hii picha ni ya cover la movie waliyocheza pamoja, Kanumba Johari na Ray, ni zawadi ambayo Marehemu Steven Kanumba alimzawadiwa baba yake, na imewekwa juu ya mlango wa kuingilia sebleni.

.

Huyu ni mdogo mwingine na Kanumba kwa upande wa baba ambae ameahidi kuingia kwenye soko la movie miaka miwili ijayo kwa sababu anaamini uwezo wa kuigiza anao.

Huyu pia ni mdogo mwingine wa Marehemu Kanumba ambae amethibitisha kwamba ana uwezo wa kuigiza, na mwaka jana alizungumza na kaka yake na alikua mbioni kumleta Dar es salaam ili kuigiza wote.

Huyu ndio mama wa hao wadogo zake Kanumba hapo juu.

.

Nyumba anayoishi Baba Kanumba na familia yake, pamoja na wapangaji.

Familia.

Kutoka kushoto ni kaka wa Marehemu Kanumba pamoja na wadogo zake kwa upande wa baba ambao wote wamekiri uwezo wa kuigiza wanao na wataingia kwenye filamu kuliendeleza jina la ukoo.

Hii ni shule aliyosoma Marehemu Kanumba, Ngokolo ni karibu na nyumbani kwa baba yake.

Wakati napita nilionyeshwa hapa kwamba ndio Nyumbani kwa kina Mwigizaji JOHARI, kumbe wanatoka sehemu moja na Kanumba, nilikua sijui.

Hili ndio kanisa la Ngokolo aliloanza kuigiza Kanumba akiwa na umri wa miaka mitano tu na alikua akiimba kwaya pia.

Hii ndio simu Kanumba aliyomnunulia baba yake mzazi mara ya mwisho kuonana june 2011, aliinunua kwa elfu 60 baada ya kukuta simu ya baba yake ni mbovu.

Hii ni nyumba ya baba Kanumba kwa nje, amepangisha watu kwenye hicho chumba cha duka pamoja na hicho kinyozi hapo kushoto.

Hii ndio Ofisi ya Marehemu Kanumba iliyopo Sinza Dar es salaam, sasa hivi inaendelea na kazi.

.

.

.

Huyo hapo kushoto ndio Zakayo Magulu, aliefanya kazi na Kanumba kwa miaka saba akiwa kama Director msaidizi, camerman na Editor.

Hii picha Kanumba ndio aliiweka ukutani kwenye duka lake.

Pembeni ya hilo duka kuna chumba cha kueditia, na pembeni Kanumba aliweka baadhi ya tuzo zake kati ya tuzo 28 alizowahi kushinda.

.

R.I.P STEVEN KANUMBA.

Kama hukupata nafasi ya kusikiliza Makala yake ya dakika 16 kuhusu mazingira ya kifo chake na mambo mengine, isikilize hapo chini……

.

Mashabiki wa shindano la Big Brother Afrika, leo tena wamepata pigo jingine baada ya Washiriki wa Nigeria, Ola na Chris kuomba kujitoa kwenye shindano hilo ambapo hiyo imetokana na Ola ambae anadaiwa kuwa mgonjwa wa bp kuwa dawa alizopewa hazijafanya kazi hivyo ni lazima atoke kwenye jumba la big brother ili kuwa karibu zaidi na matibabu ya uhakika.

Chris ambae ni mshiriki mwenzake walietoka pamoja kwenye jumba hilo, amehuzunika sana kwa kilichotokea kwa mwenzake na kukiri kwamba anaelewa, walikua kwenye mashindano wakicheza pamoja lakini hawawezi kucheza na maisha yao.

.

Baada ya ombi hilo Big Bro aliwakubalia kuondoka, na ikabidi wawaage washiriki wenzao leo leo na kuondoka japo wenzao waliwaruhuru kuondoka kutokana na hali halisi, huzuni ilitawala, washiriki wengine waliobaki walihuzunika sana na wengine hata kulia kabisa kwa sababu bado walipenda kuendelea kukaa na Chris na Ola.

Washiriki hao wawili wanakamilisha idadi ya washiriki watano walioondoka ndani ya jumba hilo kwa mwaka huu wakiwemoa watanzania wawili pamoja na mzimbabwe mmoja japo Chris na Ola wametoka bila utaratibu wa kawaida wa washiriki kutolewa kwenye jumba hilo ambapo huwa ni kila jumapili.

.

FACEBOOK YAUZA HISA ZAKE.

Posted: 19th May 2012 by MillardAyo in News

Makao makuu ya facebook California Marekani.

Kampuni ya FACEBOOK leo imeuza hisa kwa watu binafsi wanaotaka kuwa wamiliki wa mtandao huyo wa kijamii ambapo hisa moja imeuzwa dola 38 sawa na shilingi elfu 62,700 za kitanzania kikiwa ni kiasi cha tatu kikubwa kwa hisa moja kuwahi kuwepo nchini Marekani.

Hisa zote zitauzwa kwa kiasi cha dola za kimarekani Bilioni 104 ambapo baada ya kuuza hisa hizo mwanzilishi na mmiliki wa facebook Mark Zuckeberg ataweka mfukoni kitita cha dola Bilioni 19 sawa na shilingi bilioni elfu 31 za kibongo kwa kampuni hiyo aliyoianzisha miaka 8 iliyopita.

Allianz Arena, uwanja itakapochezwa fainali ya Eufa kati ya Bayern Munich na Chelsea.

Shaffih Dauda wa Sports Etra na Sports Bar ameripoti kutoka Ujerumani kwamba Ticket za bei rahisi za kuishuhudia mechi ya Chelsea na Bayern Munich Ujerumani May 19 2012 ikiwa ni fainali ya UEFA zimekwisha ambapo ticket pekee zilizobaki ni za Euro 2000 zaidi ya shilingi milioni nne za kitanzania.

Dj Mac ambae ni mbongo anaeishi Munich amesema kwa sasa bado wageni wanazidi kuingia kutoka miji na nchi mbalimbali, hali ya ticket imekua ngumu sana huku pia hata maeneo ya wazi ya kutizama mpira katika screen kubwa nayo yamejaa, mfano Olympia Stadium uwanja wa zamani wa Fc Bayern penye uwezo wa kuchukua watu elfu 30 napo Ticket zimekwisha, na pia sehemu nyingine yenye uwezo wa kuchukua watu elfu 30 kumejaa pia.

Mac amesema Kwa upande wa jezi nazo pia zimepanda sasa hivi zinauzwa kuanzia shilingi laki mbili za kitanzania ambapo mashabiki wa Bayern Munich wamehamasishwa kuvaa jezi nyeupe na nyekundu ambazo zimependezesha mji pia.

Uwanja wa Allianz Arena wakati wa mchana.

ALICHOKISEMA GODZILLA KUHUSU MAONI YA VIDEO YAKE YA KWANZA.

Posted: 18th May 2012 by MillardAyo in News

Hii ni sehemu ya hiyo video mpya ambayo imepigwa baharini kwenye boti.

Baada ya kupokea lawama kwamba video yake ya kwanza aliyoifanya haikua kama wengi walivyotarajia kutokana na ukali wa single yake ya kingzilla, Mshkaji kutoka salasala Godzilla amesema this time ameyafanyia kazi maoni aliyopata, kioo kingine anakisogeza machoni pako wiki ijayo kinaitwa hardwork pays.

Amesema video hiyo ambayo imepigwa kwenye private boat ya kifahari pamoja na boat nyingine iliyotumika kuwabeba watu wa Camera imegharimu zaidi ya milioni sita, tofauti na video yake ya mwanzo ambayo iligharimu milioni moja na nusu.

Zilla amekubali kwamba alipokea maoni ya fans wengi waliosema single ya Kingzilla haikuendana na video yake, ndio maana this time kaamua kubadilika ikiwa ni video yake ya pili toka ameanza muziki, kila kitu amepanga yeye ikiwemo mavazi na ishu nyingine.

Millard Ayo na Godzila kwenye makao makuu ya Clouds Media Group Mikocheni.

ISIKILIZE U HEARD YA MAY 18 2012 ON XXL CLOUDS FM.

Posted: 18th May 2012 by MillardAyo in News

.

U heard ya May 18 ni kuhusu wasanii wa bongo fleva kuchapwa bakora kisa wamekwenda kufanya video karibu na eneo la ibada…. isikilize mwenyewe hapo chini.