
.
Ni wizi ambao rekodi zake zinatofautiana lakini bado wengi wanalalamika kwamba magari yao yanapoibiwa kama hivi huwa hawasikii na kuna uwezekano mkubwa wezi wanatumia kimiminika cha aina flani kulainisha vioo kisha wanafungua milango.
Mkoa wa Dar es salaam ndio wenye rekodi nyingi za wizi wa aina hii, sasa hivi sio lazima gari lako liwe nyumbani au uliache sehemu kwa muda mrefu ndio litaibiwa, yani hali imebadilika kiasi kwamba wezi wa sasa wamekua wafatiliaji sana.
Wakishajua huwa unatembea na mali za gharama kama laptop, pochi, simu na vitu vingine ambavyo ni rahisi kubeba, wanakufatilia bila wewe kujua hata wiki nzima ambapo ukijisahau tu ukashuka sehemu hata dakika 5 na kuacha vitu ndani ya gari, huvikuti.

.
Zamani wamiliki wa magari walikua wanaamini gari kuwa na vioo vyeusi inasaidia mwizi kutoona kitu ndani, hivyo inakua ngumu kufikiria kuvunja… millardayo.com imepata uhakika wa mbinu nyingine inayotumika kwa mwizi kujua kama kuna mali ndani ya gari.
Wanavyo vifaa maalum ambavyo wanavipitisha nje ya gari, akipita tu nje ya gari kama uliacha kitu chochote cha umeme kile kifaa kinampa ishara kwamba hapa kuna mzigo karibu.
Cha kufanya ni kutoacha mali yoyote kwenye gari hata kama unashuka kwa dakika mbili na unaona hakuna gari lolote au mtu yeyote karibu yako au aliekuona……. mbinu nyingine waliyonayo pia ni ujanja wa kufungua mlango bila kuvunja kioo, wanatumia waya.

.

.
Kama uko Dar es salaam, pia kwenye foleni wakati wa jioni kuna wizi wa aina mbalimbali inabidi uchukue tahadhari tu… na sio kwenye foleni peke yake, kwenye sehemu zenye matuta au taa, kuna watu huwa wanajificha na kujitokeza pale tu anapoona uko mwenyewe na dirisha liko wazi au umeshika simu ambayo inatoa mwanga.
Jeshi la Polisi Kinondoni lilitoa takwimu ya mwaka huu peke yake kwa watu waliokamatwa kwa kujihusisha na wizi kama huu na hata wa kutumia pikipiki kwenye foleni au kumpokonya mtu begi akiwa anatembea barabarani ambapo ni kesi zaidi ya 30 kuanzia january mpaka feb.

.