The TZA | millardayo.com

Ombi jingine

Kwa kiasi kikubwa inaniumiza kila nikifikiria jinsi ambavyo usumbufu unajitokeza millardayo.com lakini bado sijakata tamaa, baada ya website kurudi hewani yamejitokeza matatizo mawili ambayo timu yangu bado inayashughulikia mtu wangu ili kusiwe na usumbufu tena.

Nakuomba sana radhi kwa hili mtu wangu, soon ratiba zetu zitaendelea kama kawaida.

Picha 6 za nyumba aliyonunua Jennifer Lopez

.

Nyumba yenye uzio mkubwa ndio ya J.Lo

Ni eneo la eka tatu lenye nyumba ya kifahari huko Hamptons New York ambayo imenunuliwa na mwimbaji J.Lo kwa dola za kimarekani milioni 10 ikiwa na vyumba 8 vya kulala, sparkling pool, pool house, theater, sauna, steam room and covered porches.

Hii stori imekuja wakati Marc Anthony ambae ni mume wa zamani wa J.Lo ametumia dola za kimarekani milioni mbili na nusu kununua nyumba huko Encino California Marekani.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

Magazeti 14 ya leo May 20 2013

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

Wizi wa aina hii kwenye magari bado upo

.

.

Ni wizi ambao rekodi zake zinatofautiana lakini bado wengi wanalalamika kwamba magari yao yanapoibiwa kama hivi huwa hawasikii na kuna uwezekano mkubwa wezi wanatumia kimiminika cha aina flani kulainisha vioo kisha wanafungua milango.

Mkoa wa Dar es salaam ndio wenye rekodi nyingi za wizi wa aina hii, sasa hivi sio lazima gari lako liwe nyumbani au uliache sehemu kwa muda mrefu ndio litaibiwa, yani hali imebadilika kiasi kwamba wezi wa sasa wamekua wafatiliaji sana.

Wakishajua huwa unatembea na mali za gharama kama laptop, pochi, simu na vitu vingine ambavyo ni rahisi kubeba, wanakufatilia bila wewe kujua hata wiki nzima ambapo ukijisahau tu ukashuka sehemu hata dakika 5 na kuacha vitu ndani ya gari, huvikuti.

.

.

Zamani wamiliki wa magari walikua wanaamini gari kuwa na vioo vyeusi inasaidia mwizi kutoona kitu ndani, hivyo inakua ngumu kufikiria kuvunja… millardayo.com imepata uhakika wa mbinu nyingine inayotumika kwa mwizi kujua kama kuna mali ndani ya gari.

Wanavyo vifaa maalum ambavyo wanavipitisha nje ya gari, akipita tu nje ya gari kama uliacha kitu chochote cha umeme kile kifaa kinampa ishara kwamba hapa kuna mzigo karibu.

Cha kufanya ni kutoacha mali yoyote kwenye gari hata kama unashuka kwa dakika mbili na unaona hakuna gari lolote au mtu yeyote karibu yako au aliekuona……. mbinu nyingine waliyonayo pia ni ujanja wa kufungua mlango bila kuvunja kioo, wanatumia waya.

.

.

.

.

Kama uko Dar es salaam, pia kwenye foleni wakati wa jioni kuna wizi wa aina mbalimbali inabidi uchukue tahadhari tu… na sio kwenye foleni peke yake, kwenye sehemu zenye matuta au taa, kuna watu huwa wanajificha na kujitokeza pale tu anapoona uko mwenyewe na dirisha liko wazi au umeshika simu ambayo inatoa mwanga.

Jeshi la Polisi Kinondoni lilitoa takwimu ya mwaka huu peke yake kwa watu waliokamatwa kwa kujihusisha na wizi kama huu na hata wa kutumia pikipiki kwenye foleni au kumpokonya mtu begi akiwa anatembea barabarani ambapo ni kesi zaidi ya 30 kuanzia january mpaka feb.

.

.

Picha 4 za gari alilonunua Wizkid

.

Ni staa wa Nigeria anaetajwa pia kuwa na wafuasi wengi vijana, kazaliwa july 16 1989 ambapo kama ilivyo kwa wasanii wengi, na yeye alianzia kuimba kanisani akiwa na miaka 11 na baadae kujipa jina la Lil Prinz ambalo alilibadili mwaka 2006.

Pamoja na ajira yake ya usanii iliyomfanya kuwa karibu na mastaa wa dunia kama Busta Rhymes na Wale, pesa yake pia inatokana na mlango wa dili mbalimbali uliofunguliwa kwake na makampuni makubwa kama Pepsi ambao amewahi kuonekana kwenye tangazo lao la TV.

.

Hii ni Porsche Panamera S ya mwaka 2013.

.

.

.

.

Binamu wa Diamond kuiwakilisha Tz BBA 2013?

.

.

Wiki iliyopita hii ndio iliingia kwenye Top 10 ya AMPLIFAYA Clouds FM kama stori iliyozungumziwa na Watanzania sana kwa wiki nzima sehemu mbalimbali kuanzia mitaani mpaka kwenye mitandao ya kijamii.

Rommy Jones alipopata nafasi ya kuongea kwenye exclusive interview na millardayo.com amesema ni kweli hizo stori zimekuepo lakini yeye mwenyewe hana uhakika kama atashinda kwenda BBA 2013 na mpaka sasa hajajua kitakachotokea.

“kushiriki nilishiriki ila sina uhakika manake sijapigiwa simu na Multichoice wala BBA kuhusu mimi kushinda, napenda kwenda…. ikitokea nimekwenda nitafurahi manake ni hela zile pia” – Rommy

Rommy ambae ameshiriki usahili wa BBA kwa mara ya kwanza mwaka huu, amewahi kufanya kazi Clouds Tv lakini pia ukaribu wake na mastaa mbalimbali wa Tanzania umemfanya kujulikana kwenye kona kibao ndani ya ardhi ya JK.

Taarifa zilizosambaa kuanzia wiki iliyopita zimeamplfy kwamba Rommy alikwenda South Afrika siku kadhaa zilizopita kwa ajili ya usahili mwingine wa mwisho kabla ya kuingia BBA huku stori nyingine pia zikimtaja msanii wa kike ambae jina lake linaanza na herufi F, kwamba na yeye anaiwakilisha Tanzania mwaka huu.

Pamoja na kwamba hizi ndio stori zinazozungumzwa sana na baadhi ya Watanzania, bado hakuna uhakika kama kweli hawa ndio wanaiwakilisha Tanzania.. tusubirie siku yenyewe

.

Rommy kwenye interview na host wa Amplifaya na Top 20 za Clouds FM, Millard Ayo

.

.

.

.

.

Rommy Jones akiwa na Diamond toka utotoni mpaka hapa walipo

Kwa mujibu wa afisa uhusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi, ni zaidi ya watu 100 waliojitokeza kwenye usahili ambapo watu maarufu ni zaidi ya watano.

Mshindi wa BBA 2013 atachukua USD 300000.

Unataka kuwa wa kwanza kupata exclusive za Tanzania? kuwa mwanafamilia wa nguvu kwa kuungana na facebook.com/millardayo twitter.com/millardayo na instagram.com/millardayo

Kwako mtu wangu wa nguvu!

Ni kwa zaidi ya wiki moja millardayo.com haikua inapatikana, hii ni kutokana na tatizo la kiteknolojia ambalo ni kubwa kuwahi kutokea kwenye hii website ambayo kwa sasa imerudi kwenye hali yake ya kawaida, asante kwa uvumilivu mtu wangu wa nguvu.

Millard Ayo.