Bohari ya Dawa (MSD) imeanza usambazaji wa vifaa tiba majimboni,vifaa hivyo vilivyonunuliwa na serikali vina thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 14.7 kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati lengo ni kupunguza vifo vya mama na mtoto.
Meneja wa MSD, Kanda ya Mashariki yenye mikoa ya Dar es Salaam, Pwani ,Morogoro na Visiwani Zanzibar, Betia Kaema alisema hayo wakati wa makabidhiano wa vifaa hivyo na mkuu wa mkoa wa Morogoro , Adam Malima kwa ajili ya majimbo 11 ya mkoa huo.
Kaema alisema , mkoa wa Morogoro umepatiwa vifaa aina tisa vyenye thamani ya sh milioni 759 na kuanza kusambazwa katika majimbo yote 11 na kila jimbo litapokea vifaa vyenye thamani ya Sh milioni 69.
“ Kama tunavyofahamu Serikali yetu inayoongozwa na Rais Mama Samia Suluhu Hassan , imenunua vifaa kwa ajili ya kupunguza vifo vya mama na mtoto vyenye thamani ya sah bilioni 14.7 na vifaa hivyo vilizinduliwa na Waziri wetu wa Afya kwa ajili ya majimbo ya Tanzania nzima” alisema Kaema.
Kaema alivitaja vifaa vilivyokabidhiwa kwa kila jimbo la mkoa huo na idadi yake kwenye mabano ni Drip stand (330), vitanda vya kawaida vya wagonjwa (330), vitanda vya kujifungulia mama wanajawazito (220) na seti (220) za kujifungulia mama wajawazito.
Alitaja vingine ni shuka (1,320), magodoro (330), Examination table (220), meza ndogo za wagonjwa kuwekea vifaa vyao pale wanapokuwa wamelazwa (165) na Bed side Locker (330).