Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, Saad Mtambule, ameongoza operesheni maalumu ya kuhamasisha matumizi na umuhimu wa risiti na stempu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Operesheni hiyo kabambe imeshirikisha maofisa wa TRA kutoka Mikoa ya Kikodi wilayani humo ambapo amewataka wafanyabiashara kuanza kuchunguza bidhaa zao walizonazo kabla ya rungu zito kuwashukia.
DC Mtambule amesema “Wale wote ambao wana bidhaa zisizo na stempu hiyo ya TRA waziondoe wenyewe katika mfumo wa biasharaa, tutawasaka na kuwakamata na hatua kali zinachukuliwa juu yao kwani wanaujumu uchumi wa nchi yetu”.
Hata hivyo naye Meneja wa TRA Mkoa wa Kikodi wa Kinondoni, Dickson Qanyara, amewataka wafanyabiashara ambao bado hawaja sajili biashara zao kufika katika ofisi za mamlaka hiyo kupata usajili sambamba na kufuata sheria na taratibu zote za msingi kabla ya operesheni kuanza kwani haitakuwa na msahama rahisi.