Serikali ya Marekani kwa Kushirikiana na Wizara ya Afya na PO-RALG watuimia ‘Ndondo CUP 2024’ Kukuza Huduma za VVU na Chanjo
Marekani, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) nchini Tanzania, imetangaza ushirikiano na mashindano ya Ndondo Cup 2024 kupitia kampeni zake mashuhuri za ‘SITETEREKI’, ‘FURAHA YANGU’ na ‘CHANJO NI MAISHA’ ili kuchochea huduma za VVU na chanjo. Mashindano haya yatafanyika katika mikoa nane nchini Tanzania, ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Pwani na Kagera.
Ushirikiano huu wa kibunifu utatekelezwa katika ngazi za kitaifa na jamii, kwa kutumia michezo kuwahamasisha vijana na wanaume wa umri wa kati kutafuta na kutumia huduma za VVU na chanjo. Ushirikiano huu utazingatia mambo muhimu kama kuelewa hatari, kujiamini, kuleta mitazamo chanya, kuunga mkono kanuni za kijamii, kuhamasisha uchukuaji wa hatua, na kuhakikisha huduma zinapatikana kwa urahisi. Lengo la mashindano haya ni kuleta mabadiliko ya kudumu ya tabia.
Ushirikiano huu utatekelezwa kwa awamu tatu: kabla, wakati, na baada ya mechi, ukijumuisha mijadala ya VVU na chanjo katika muktadha wa mpira wa miguu na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za afya katika maeneo muhimu. Jitihada hizi zinawakilisha hatua muhimu katika kuendesha mabadiliko chanya ya tabia kuhusu VVU na chanjo na kuongeza matumizi ya huduma hizi.
“Tumejitolea kubuni mbinu zinazotoa matokeo halisi ya kiafya,” alisema Evangelina Chihoma kutoka Ofisi ya PEPFAR. “Tunaamini kwamba michezo inaweza kuongeza nguvu kubwa katika kuleta mabadiliko ya tabia na kuboresha upatikanaji wa huduma, na tunafurahia kushirikiana na Ndondo Cup na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufanikisha mashindano haya.”
Ndondo Cup 2024 ni hatua muhimu katika kuchochea upatikanaji wa huduma muhimu za afya nchini Tanzania, na inakuza tabia za kiafya na matumizi ya huduma miongoni mwa vijana wa kiume na wanaume wenye umri wa kati.
Kwa maelezo zaidi, tafadhali wasiliana na Ofisi ya Habari ya Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam kupitia DPO@state.gov.