Watanzania wametakiwa kuunga mkono juhudi za Rais Dk Samia Suluhu Hassan katika nyanja ya elimu ambayo ameelezwa kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika sekta hiyo.
Wito huo umetolewa na mwanafunzi Ayla Amalile mwenye umri wa miaka 17 ambae ameunga mkono juhudi za mheshimiwa Rais kwa kukarabati madarasa mawili ambayo yalikuwa na hali mbaya katika shule ya msingi Kiwawa kata ya Imbaseni Hs Meru kwa kutumia fedha zake za matumizi ya shule zaidi ya shilingi milioni tatu.
Ayla amesema anatambua umuhimu wa mwanafunzi kusoma kwenye mazingira bora ndio maana aliguswa kuunga mkono juhudi za mheshimiwa rais ambae amesema amekuwa ni mwanamke wa mfano.