Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, amemjibu Rais wa Marekani wa wakati huo, Donald Trump, baada ya Trump kutangaza kusitisha misaada kwa taifa hilo akidai kuwa kuna ukiukwaji wa haki za binadamu, pamoja na madai kuwa Wazungu wananyanyaswa na kupokonywa ardhi wanazomiliki.
Akijibu madai hayo, Ramaphosa amemtaka Trump aache kuingilia masuala ya ndani ya Afrika Kusini kwa kuwa hayamhusu. Amesisitiza kuwa ardhi ya Afrika Kusini ni ya raia wa nchi hiyo, na Trump hana mamlaka ya kuwapangia cha kufanya.
“Hii ni ardhi yetu, sijui Donald Trump anahusika vipi au atafanya nini kuhusu ardhi ya Afrika Kusini kwa sababu hajawahi kuwa hapa. Aitunze Marekani yake, nasi tutaitunza Afrika Kusini yetu. Afrika Kusini ni ardhi yetu na inamilikiwa na watu wote wanaoishi hapa, siyo ya Trump,” amesema Ramaphosa.
Tazama zaidi…