TANZANIA inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Tatu wa (G25 African Coffee Summit) kwa Nchi zinazolima kahawa Afrika, utakaofanyika Februari 21 na 22, 2025, katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere, Jijini Dar es Salaam.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa, Primus Kimaryo, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea mkutano huo wa Wakuu wa Nchi za Afrika zinazolima kahawa.
Kimaryo alifafanua kuwa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano huo, ambapo zaidi ya washiriki 1,500 wanatarajiwa kushiriki ili kujadili masuala mbalimbali ya sekta ya kilimo, hususan kilimo cha kahawa.