Hawa ndio Watanzania wawili waliotajwa na CNN kuwania Tuzo ya Wajasiriamali chini ya Miaka 23 Africa..
Share
6 Min Read
SHARE
Kuna Tuzo zinaitwa ANZISHA AWARDS, nimezifahamu leo baada ya kukuta kuna majina wa Watanzania wawili ambao wametajwa kwenye vijana 12 waliotajwa kuwania Tuzo hizo mwaka 2015.
Tuzo hizo zimeanzishwa kwa ajili ya kuwatambua na kuwatuza Vijana wenye umri wa kati ya miaka 17 na 22 ambao wanajihusisha na ujasiriamali na kupitia ujasiriamali wao wamesaidia kubuni miradi ambayo inatatua baadhi ya changamoto za Kijamii.
Kwenye majina ya Vijana 12 waliotajwa kuwania Tuzo hizo wako pia Watanzania wawili, George Mtemahanjimwenye umri wa miaka 22 na Sirjeff Dennisambaye ana miaka 21.
Vijana wote 12 hawa hapa.
Huyu niGeorge Mtemahanji, Mtanzania ambaye ameingia kwenye Tuzo hizo baada ya kuanzisha mradi wa umeme wa Jua na Kampuni yake inaitwaSunSweat Solar Limited, Kampuni yake inahudumia watu waishio Vijijini ambako kuna tatizo kubwa la umeme.Mtanzania mwingine ni huyu,Sirjeff Dennis… yeye nae yumo, Mradi alioanzisha ni wa kukabiliana na Changamoto ya ukosefu wa Chakula pamoja na umaskini Vijijini, kupitia ufugaji wa Kuku na Kilimo cha mbogamboga. Jamaa pia ana Kampuni yake ambayo kaipa jina laJefren Agrifriend Solutions, Biashara yake kubwa ni kuuza Kuku na Mayai.Fabrice Alomo, kijana waCameroonambaye ameanzisha Website yaMyAConnectambayo inasaidia Wafanyabishara wadogowadogo kuuza bidhaa kwa njia ya Mtandao.Mabel Suglo, huyu ni kijana wa Ghanaambaye naye ameingia kwenye list ya vijana hao 12, yeye aliguswa na nafasi ya watu wenye ulemavu kwenye Jamii.. akaona aanzishe kitu kinaitwaEco-Shoes Projectambapo aliowaajiri kufanya kazi ya kutengeneza viatu ni watu wenye ulemavu… Viatu vinatengenezwa kwa Matairi na nguo ambazo zimechakaa na hazifai kuvaliwa.Huyu anaitwaFarai Munjoma, kijana kutoka Zimbabwe, yeye kaanzisha Shasha Iseminar ambayo pia ni system ya kujisomea Mtandaoni na sehemu ya mapato anayoyapata anasaidia pia kulipia ada baadhi ya Wanafunzi ambao wazazi wao hawana uwezo Vijijini.Vanessa Zommi… huyu mrembo anatoka Cameroonna umri wake ni miaka 19 tu, lakini alianzisha Kampuni ya Emerald Moringa Tea, ambayo inatengeneza majani ya Chai yanayosaidia kufanya mfumo wa Chakula mwilini kuwa vizuri, unaambiwa majani anayotengeneza ni ya kutokana na mmea ambao Cameroon wanauita Moringa.Huyu ni Mnigeria,Chris Kwekoweambaye alianzisha System ya kujisomea Mtandaoni ambayo inaitwaSlatecubena kusaidia hata wasio na uwezo wa kulipia gharama za Vyuo kujisomea Mitandaoni kwa urahisi kabisa.Daniel Mukisa kutokaUganda. Daniel bado ni Mwanafunzi waChuo Kikuu cha Makerere, ameanzisha mradi wa Usafirishaji kwa kutumia Baiskeli, aliona kuna ishu ya foleni na pia Barabara mbovu kwenye maeneo mengi, mradi wake unalenga kufikisha bidhaa mpaka nyumbani kwa wateja ambao wamenunua bidhaa kwa njia ya Mtandao, kwa baiskeli bidhaa zinawafikia wateja kwa haraka na inasaidia pia kuokoa gharama za usafirishaji.Chantal Butare, mrembo mwingine kutoka Rwanda ambaye alianzishaKinazi Dairy Cooperative, mradi ambao unawasaidia Wafugaji wadogowadogo 3,200 kuuza maziwa ya ng’ombe wao. Soko la maziwa hayo liko ndani yaRwanda na Burundi na kazi ya kuuza inasimamiwa na huyu mrembo.Karidas TshintsholokutokaSouth Africa… nae yumo kwenye Washiriki 12 waliopita kuingia kwenye Tuzo hizo, yeye ana mradi waPush Imsokol Clothingambapo anajihusisha na kutengeneza T-shirt, Kofia na Masweta ambayo yana soko zuri ndani ya South Africa.Hidaya Ibrahim kutokaEthiopia, huyu ndiye Mwanzilishi waQine Association for Promoting Education Qualityambayo inajumuisha pamoja Taasisi za Elimu Shule za Serikali na Shule Private pamoja na Wanafunzi wao katika kutatua Changamoto za ElimuEthiopia.Blessing Fortune Kwomo kutokaNigeria. Mazingira aliyokulia yalikuwa ni magumu kiasi cha kwamba kuna wakati alikuwa akiumwa na Familia yake ilishindwa kumudu gharama za matibabu, kwa sasa ni Mwanafunzi wa Utabibu na ameanzishaDe Rehoboths Therapeutic Studioambayo inahudumia Majumbani baadhi ya watu wenye matatizo ya kiafya na hawana uwezo.
Hao ndio Washiriki wote kwenye Tuzo hizo ambao wanawakilisha jumla ya Nchi tisa za Africa, Washindi watapatikana Mwezi November 2015 ambapo zawadi itakayotolewa mwaka huu ni Dola 75,000/= kwa washindi watatu, kila mmoja Dola 25,000/= ambayo ni sawa na Milioni 54 za Kitanzania.
Unataka kutumiwa MSG za habari zote kubwa kutoka kwa Millard Ayo? ukiwa na line ya tiGO andika ‘AYO’ tuma kwenda 15510, msg utayotumiwa jibu OK ili uanze kupokea matukio yote kwa sms, pia ungana na Millard Ayo kwenye Twitter, FB, Instagram na YouTUBE kwa kubonyeza hapa>>>INSTAGRAM,TWITTER,FB,YOUTUBE