Wanawake wengi wanaopenda kushiriki urembo huwa wakawamekuwa wakitumia chakula kidogo sana na wengine kujinyima kula kabisa ili kufanya miili yao ibaki kuwa midogo, lengo likiwa kutimiza nia yao ya kushiriki mashindano mbalimbali ya urembo.
Hii ishu ni kama imenishtua hivi, mwanaume kufanya jitihada ili aote maziwa kama mwanamke na aende kushiriki mashindano ya Urembo.. Juan Sanchez ni raia wa Mexico, lengo lake la kujiongeza maziwa halikufanikiwa.. alijichoma sindano ya mafuta kifuani ili awe na maziwa kama mwanamke, yale mafuta yalikuwa na sumu ambayo ilisambaa kwenye mapafu na ubungo na baadae alifariki.

Baada ya kujichoma sindano hiyo alianza kuumwa, marafiki zake wakampeleka hospitali ya jirani ambapo alipofika daktari alisema dawa aliyotumia ilikuwa sumu ambayo ilisambaa kwenye ubongo na mapafu na ndiyo iliyomsababishia kifo siku nane tu baada ya kujichoma sindano hiyo.
Unahitaji chochote ninachokipata kisikupite? jiunge na mimi kwenye Twitter, Facebook na Instagram kwa kubonyeza hapa >>> Twitter Insta FB na nitakua nikikutumia kila ninachokipata pia usisahau kusubscribe YouTube kwa kubonyeza hapa >>>Videos ili kila video ya AyoTV ikufikie.