Maadhimisho ya kitaifa ya Kiswahili yanatarajiwa kufanyika siku ya terehe 7 ya mwezi huu jijini Dar es Salaam huku maadhimisho hayo yakitegemewa kwenda sanjari na matembezi maalumu ili kuhamasisha usomaji vitabu hususani vya kiswahili.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Bi, Consolata Mushi amesema maadhimisho ya Kiswahili yataanza tarehe tano kwa matembezi maalumu yatakayoongozwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam akiwa na wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Kuhusu maadhimisho ya kimataifa ya Kiswahili Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Bi, Consolata Mushi amesema “maadhimisho hayo yatafanyika tarehe saba katika ukumbi wa mwalimu nyerere ambapo viongozi mbalimbali wakuu wa serikali watashiriki”.
Hata hivyo amesema kwa sasa mijadala mbalimbali ya kitaalamu kuhusu Kiswahili inaendelea katika maeneo mbalimbali huku akiwataka watanzania kuendelea kuunga mkono lugha ya Kiswahili.