Pichaz za utoaji wa Tuzo za TASWA 2015 na Rais Jakaya Kikwete akipewa Tuzo ya heshima
Share
4 Min Read
SHARE
Hatimaye lile tukio la utolewaji wa Tuzo za chama cha waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) ambazo hutolewa kila mwaka kwa wanamichezo wanaofanya vizuri, zimekamilika usiku wa October 12 kwa wanamichezo, taasisi na viongozi waliofanya vizuri katika kipindi cha miaka 10, Tuzo hizo safari hii zimekuwa tofauti na miaka yote kwani waliopewa Tuzo ni wale waliofanya vizuri katika kipindi cha miaka kumi.
Shadrack Nsajigwa akipokea Tuzo kwa niaba ya timu iliyofanya vizuri katika mashindano ya CHAN
Tuzo hizo ambazo zilikuwa maalum mwaka huu, kwani zimetumika kumuaga Rais Kikwete kwa kumaliza muda wake madarakani na kuheshimu mchango wake katika kuinua michezo nchini katika kipindi cha utawala wake. Ikumbukwe kuwa Tuzo hizo ziligawanyika katika vipengele vinne, Taasisi iliyochangia kuinua michezo katika kipindi cha miaka kumi Tuzo 5.
Francis Cheka akipokea Tuzo yake
Tuzo zimetolewa kwa wanamichezo waliofanya vizuri katika kipindi cha miaka kumi, viongozi waliochangia kuinua michezo katika kipindi cha miaka kumi Tuzo 5 na Tuzo ya heshima kwa Mh Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuheshimu mchango wake katika kuinua michezo wakati wa utawala wake, baadhi ya waliopewa Tuzo usiku wa October 12 ni Francis Cheka, Mbwana Samatta, Iddi Kipingu, Abdallah Majura na Hasheem Thabeet
Mama yake Hasheem Thabeet akichukua Tuzo kwa niaba ya Hasheem
Charles Mkwasa akichukua Tuzo ya Twiga Stars kwa kufanya vizuri katika kipindi cha miaka 10.Wawakilishi wa Mbwana Samatta wakichukua Tuzo kwa niaba yake
Kanali Iddi Kipingu akipokea Tuzo yake ya heshima kwa kusaidia kuinua michezo kwa muda mrefu toka yupo shule ya MakongoRais Kikwete akimkabidhi tuzo Dioniz Malinzi kwa kujenga Uwanja wa Gofu Misenyi mkoani KageraRais wa zamani wa TFF Leodger Tenga kapata Tuzo ya kiongozi bora katika kuinua michezoAbdallah Majura akikabidhiwa Tuzo ya heshima katika kuinua michezo sasa kafungua kituo cha Radio kinachojihusisha na michezo.Mzee Said akipokea Tuzo ya Taasisi iliyochangia kuinua michezo nchini Azam SSBMwenyekiti wa TASWA Juma Pinto akimkabidhi Rais Kikwete Tuzo ya heshima akiwa pamoja na mkuu wa mkoa Dar Es Salaam Said Meck Sadick, waziri wa michezo Dk Fenella Mukangara na Dioniz Malinzi.
Nahodha wa Taifa Stars Nadir Haroub akikabidhi jezi ya Taifa Stars kwa Rais Kikwete ikiwa imesainiwa na wachezaji wote.Baada ya ugawaji wa Tuzo Rais Kikwete alipata nafasi ya kuongea na waandishi wa habari na wageni waalikwa katika Tuzo hizo.
Rais Kikwete katika picha ya pamoja na watu mbalimbaliRais Kikwete katika picha ya pamoja na washindi wa Tuzo hizoYamoto Band wakaitimisha kwa kuwachezesha waandishi wa habari kimadoido
Unataka kutumiwa MSG za habari zote kubwa kutoka kwa Millard Ayo? ukiwa na line ya tiGO andika ‘AYO’ tuma kwenda 15510, msg utayotumiwa jibu OK ili uanze kupokea matukio yote kwa sms, pia ungana na Millard Ayo kwenyeTwitter,FB,Instagram na YouTUBE wa kubonyeza hapa >>>INSTAGRAMTWITTERFBYOUTUBE.